Niliwahi kuelezwa hapo kitambo ya kwamba kuna mtu ambaye alikuwa hawatoi wasichana wake wakubwa kuwaoza. Mmoja wao akaumwa. Pengine vilevile aliugua kwa sababu ya kuzuiwa kuolewa – Allaah ndiye mjuzi zaidi ya hili. Kabla ya kukata roho na mbele yake kulikuwa wanawake wengine, akawapa ujumbe:
“Mwambieni baba yangu miadi yangu mimi na yeye ni siku ya Qiyaamah nitaposimama nae mbele ya Allaah.”
Namna hii ndio alimwambia baba yake. Hata kama asingemwambia hivi huu ndio uhakika wa mambo. Hata kama asingemwambia hivi mwanamke huyu atakuwa mgomvi wake siku ya Qiyaamah ambayo kila mmoja atamkimbia mwenzie.
Nasaha zangu kwa walezi wa wanawake: wamche Allaah (´Azza wa Jall) na wasiwazuie wanawake kwa wale ambao ni haki kwao kuwaoza kwa ambaye kumeridhiwa juu yake dini na tabia yake. Ana haki ya kumkatalia ikiwa atamchagua ambaye hana dini na tabia. Lakini amemchagua mwanaume ambaye ana dini njema na tania nzuri kisha akamkatalia pasi na sababu, ni kitendo cha haramu, dhambi na khiyana. Sababu yoyote itayopelekea akaharibika madhambi anapata yeye – yaani huyu mlezi wake.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (07)
- Imechapishwa: 01/05/2020
Niliwahi kuelezwa hapo kitambo ya kwamba kuna mtu ambaye alikuwa hawatoi wasichana wake wakubwa kuwaoza. Mmoja wao akaumwa. Pengine vilevile aliugua kwa sababu ya kuzuiwa kuolewa – Allaah ndiye mjuzi zaidi ya hili. Kabla ya kukata roho na mbele yake kulikuwa wanawake wengine, akawapa ujumbe:
“Mwambieni baba yangu miadi yangu mimi na yeye ni siku ya Qiyaamah nitaposimama nae mbele ya Allaah.”
Namna hii ndio alimwambia baba yake. Hata kama asingemwambia hivi huu ndio uhakika wa mambo. Hata kama asingemwambia hivi mwanamke huyu atakuwa mgomvi wake siku ya Qiyaamah ambayo kila mmoja atamkimbia mwenzie.
Nasaha zangu kwa walezi wa wanawake: wamche Allaah (´Azza wa Jall) na wasiwazuie wanawake kwa wale ambao ni haki kwao kuwaoza kwa ambaye kumeridhiwa juu yake dini na tabia yake. Ana haki ya kumkatalia ikiwa atamchagua ambaye hana dini na tabia. Lakini amemchagua mwanaume ambaye ana dini njema na tania nzuri kisha akamkatalia pasi na sababu, ni kitendo cha haramu, dhambi na khiyana. Sababu yoyote itayopelekea akaharibika madhambi anapata yeye – yaani huyu mlezi wake.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (07)
Imechapishwa: 01/05/2020
https://firqatunnajia.com/nasaha-kwa-wazazi-wasiotaka-kuwaoza-mabanati-wao/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)