Swali: Ni vipi nimtendee mama yangu wema baada ya kufa kwake?
Jibu: Imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba aliulizwa na mtu ambaye alisema: “Ee Mtume wa Allaah! Kumebaki kitu katika kuwatendea wema wazazi wangu ninachoweza kuwatendea baada ya kufa kwao?” Akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kuwaombea du´aa, kuwaombea msamaha, kuwatimizia ahadi zao, kuwakirimu marafiki zao, kuwaunga jamaa zao wa lazima.”
Yote haya ni katika kuwatendea wema wazazi baada ya kufa kwao.
Kwa hivyo tunakuusia kuwaombea du´aa, msamaha na kutekeleza wasia wa mama yako unaokubaliki katika Shari´ah. Aidha wakirimu marafiki zake, waunge wajomba, shangazi na jamaa zako wengine upande wa mama yako.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ajmuu´-ul-Fataawaa (09/295)
- Imechapishwa: 17/07/2021
Swali: Ni vipi nimtendee mama yangu wema baada ya kufa kwake?
Jibu: Imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba aliulizwa na mtu ambaye alisema: “Ee Mtume wa Allaah! Kumebaki kitu katika kuwatendea wema wazazi wangu ninachoweza kuwatendea baada ya kufa kwao?” Akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kuwaombea du´aa, kuwaombea msamaha, kuwatimizia ahadi zao, kuwakirimu marafiki zao, kuwaunga jamaa zao wa lazima.”
Yote haya ni katika kuwatendea wema wazazi baada ya kufa kwao.
Kwa hivyo tunakuusia kuwaombea du´aa, msamaha na kutekeleza wasia wa mama yako unaokubaliki katika Shari´ah. Aidha wakirimu marafiki zake, waunge wajomba, shangazi na jamaa zako wengine upande wa mama yako.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: ajmuu´-ul-Fataawaa (09/295)
Imechapishwa: 17/07/2021
https://firqatunnajia.com/namna-ya-kumtendea-mzazi-wema-baada-ya-kufa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)