Swali: Inajuzu kwa mke kuchukua pesa kutoka kwa mume bila ya mume wake kujua pamoja na kuzingatia ya kwamba anamjali na anampa mahitajio yake yote? 1.15
Jibu: Hapana. Ikiwa anamsimamia matumizi ya wajibu, basi asichukue chochote pasi na idhini yake. Ama ikiwa anapunguza kitu katika matumizi na hampi wakati anapomuomba, achukue kiwango tu kile kinachomtesheleza. Hind bint ´Utbah (Radhiya Allaahu ´anhaa) alisema:
“Ee Mtume wa Allaah! Abu Sufyaan ni mwanaume bakhili. Ni dhambi nikuchukua mali yake kwa ajili ya kulisha familia yetu?” Akamwambia: “Hapana, chukua kinachokutosheleza kwa wema.”[1]
Ikiwa mtu hapati haki yake kutoka kwa mtu anayeipinga au anayechelewesha kulipa deni, achukue haki yake.
[1] Muslim (1714).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (63) http://alfawzan.af.org.sa/node/16495
- Imechapishwa: 26/08/2017