Makusudio ya الرفيق الأعلى

Swali: Nini maana ya msemo:

لحق بالرفيق الأعلى

“Nikutanishe na waja walio katika daraja za juu.”

kabla ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kukata roho?

Jibu: Waja walio katika daraja za juu ni Mitume, Manabii na waja wengine wema ambao Allaah (Jalla wa ´Alaa) amesema juu yao:

وَمَن يُطِعِ اللَّـهَ وَالرَّسُولَ فَأُولَـٰئِكَ مَعَ الَّذِينَ أَنْعَمَ اللَّـهُ عَلَيْهِم مِّنَ النَّبِيِّينَ وَالصِّدِّيقِينَ وَالشُّهَدَاءِ وَالصَّالِحِينَ ۚ وَحَسُنَ أُولَـٰئِكَ رَفِيقًا

“Atakayemtii Allaah na Mtume, basi hao watakuwa pamoja na wale Allaah aliowaneemesha miongoni mwa Manabii na wakweli na mashahidi na waja wema – na uzuri ulioje kuwa pamoja na hao.”[1]

Wakati wa kufa pia akasema:

اللهم في الرفيق الأعلى

“Ee Allaah! Waja walio katika daraja za juu.”[2]

Kwa sababu hawa ndio waja walio katika daraja za juu ambao wamekwishaingia Peponi na kuwa ndani yake miongoni mwa Mitume na wafuasi wao. Hivyo anamwomba Mola Wake awe pamoja nao wema hawa ambao wamemtii Allaah na Mtume Wake na hivyo wakawa katika Pepo. Hawa ndio waja walio katika daraja za juu waliolengwa katika maneno Yake (Ta´ala):

وَمَن يُطِعِ اللَّـهَ وَالرَّسُولَ فَأُولَـٰئِكَ مَعَ الَّذِينَ أَنْعَمَ اللَّـهُ عَلَيْهِم مِّنَ النَّبِيِّينَ وَالصِّدِّيقِينَ وَالشُّهَدَاءِ وَالصَّالِحِينَ ۚ وَحَسُنَ أُولَـٰئِكَ رَفِيقًا

“Atakayemtii Allaah na Mtume, basi hao watakuwa pamoja na wale Allaah aliowaneemesha miongoni mwa Manabii na wakweli na mashahidi na waja wema – na uzuri ulioje kuwa pamoja na hao.”

Tunamuomba Allaah nasi atujaalie kuwa miongoni mwao.

[1] 04:69

[2] Tazama https://firqatunnajia.com/48-duaa-ya-mgonjwa-ambaye-amekataa-tamaa-ya-kuishi-tena/

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1572/%D8%A8%D9%8A%D8%A7%D9%86-%D9%85%D8%B9%D9%86%D9%89-%D9%82%D9%88%D9%84%D9%87-%D9%84%D8%AD%D9%82-%D8%A8%D8%A7%D9%84%D8%B1%D9%81%D9%8A%D9%82-%D8%A7%D9%84%D8%A7%D8%B9%D9%84%D9%89
  • Imechapishwa: 01/05/2020