Kusema “Allaahu Akbar” mahala pa kupanda na “Subhaana Allaah” mahala pa kushuka

Swali: Mtu akipanda kwenye daraja au lifti imependekezwa kwake kusema “Allaahu Akbar” na anaposhuka mahala kusema “Subhaana Allaah” mbali na safari?

Jibu: Hili ni jambo zuri. Yote haya ni Dhikr na ni jambo zuri. Yote yanahusiana na kupanda na kushuka – hata kama asli yake ni katika safari.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (35) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/mo–1431-11-09.mp3
  • Imechapishwa: 15/11/2014