Swali: Ni upi usahihi wa Hadiyth:

“Yule mwenye kuinusuru batili ilihali anaijua hatoacha kuwa katika Hasira za Allaah mpaka aache aliyoyasema”?

Jibu: Nijualo ni kwamba Hadiyth ni Swahiyh. Tunamuomba Allaah afya. Tumeona wengi katika watu katika wakati huu wanajua haki na wanaipiga vita na wanawapiga vita watu wake na wanainusuru batili na wanasaidia kuinusuru batili na wanaidhibiti batili na watu wake na wanawapandisha mpaka katika daraja ya mashahidi na Mujaahiduun na kadhalika katika sifa zingine ambazo wanawasifu kwazo Ahl-ul-Baatwil na Ahl-ul-Bid´ah.

Jambo hili ni khatari. Allaah Hatoacha kuwa na Hasira na yeye mpaka aache aliyoyasema. Tunamuomba Allaah Atuwafikishe sisi na wao kuachana na upotevu huu na na kuunusuru.

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.rabee.net/show_fatwa.aspx?id=136
  • Imechapishwa: 09/08/2020