Swali: Niliswali na imamu na nilikuwa nimekuja nimechelewa Rak´ah moja. Imamu alipotoa Tasliym nami nikatoa Tasliym hali ya kusahau. Papo hapo baada ya swalah nilipokumbuka nikakamilisha swalah yangu. Lakini sikusujudu sijda ya kusahau. Je, juu yangu kuna kitu?
Jibu: Ikiwa uliacha sijda ya kusahau kwa makusudi, basi swalah yako ni batili. Na ikiwa uliiacha kwa kusahau, basi unatakiwa kusujudu pale utakapokumbuka na hivyo swalah yako ni sahihi. Ingawa baadhi ya wanazuoni wanaona kuwa kukishapita muda kitambo kirefu au wudhuu´ wako ukachenguka basi sijda [ya kusahau] inadondoka.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (21)
- Imechapishwa: 08/08/2021
Swali: Niliswali na imamu na nilikuwa nimekuja nimechelewa Rak´ah moja. Imamu alipotoa Tasliym nami nikatoa Tasliym hali ya kusahau. Papo hapo baada ya swalah nilipokumbuka nikakamilisha swalah yangu. Lakini sikusujudu sijda ya kusahau. Je, juu yangu kuna kitu?
Jibu: Ikiwa uliacha sijda ya kusahau kwa makusudi, basi swalah yako ni batili. Na ikiwa uliiacha kwa kusahau, basi unatakiwa kusujudu pale utakapokumbuka na hivyo swalah yako ni sahihi. Ingawa baadhi ya wanazuoni wanaona kuwa kukishapita muda kitambo kirefu au wudhuu´ wako ukachenguka basi sijda [ya kusahau] inadondoka.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (21)
Imechapishwa: 08/08/2021
https://firqatunnajia.com/hukumu-ya-kuacha-sijda-ya-kusahau/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)