Swali: Je, mtu anapata thawabu za kufunga siku sita za Shawwaal ikiwa ana deni kabla ya kumaliza kulipa deni lake la Ramadhaan?
Jibu: Mtu halipwi thawabu za kufunga siku sita za Shawwaal ikiwa hajakamilisha Ramadhaan nzima. Kwa yule mwenye deni la Ramadhaan basi asifunge siku sita za Shawwaal mpaka kwanza akamilishe Ramadhaan nzima, kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayefunga Ramadhaan kisha akaifuatishia siku sita za Shawwaal basi ni kama ambaye amefunga mwaka mzima.”
Kutokana na hili tunasema kumwambia yule mwenye deni kwanza aanze kufunga deni lake kisha ndio afunge siku sita za Shawwaal. Shawwaal ikimalizika kabla ya kuwahi kufunga hizo siku sita, basi thawabu zake zinapotea isipokuwa kama amechelewesha kwa udhuru. Mtu akijaaliwa kufunga siku sita hizo kila jumatatu na alkhamisi basi analipwa thawabu mara mbili kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika kila kitendo kinategemea na nia na kila mmoja atalipwa kutokana na vile alivyonuia.”[1]
[1] al-Bukhaariy (1) na Muslim (1907).
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (20/18-19)
- Imechapishwa: 06/06/2019
Swali: Je, mtu anapata thawabu za kufunga siku sita za Shawwaal ikiwa ana deni kabla ya kumaliza kulipa deni lake la Ramadhaan?
Jibu: Mtu halipwi thawabu za kufunga siku sita za Shawwaal ikiwa hajakamilisha Ramadhaan nzima. Kwa yule mwenye deni la Ramadhaan basi asifunge siku sita za Shawwaal mpaka kwanza akamilishe Ramadhaan nzima, kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayefunga Ramadhaan kisha akaifuatishia siku sita za Shawwaal basi ni kama ambaye amefunga mwaka mzima.”
Kutokana na hili tunasema kumwambia yule mwenye deni kwanza aanze kufunga deni lake kisha ndio afunge siku sita za Shawwaal. Shawwaal ikimalizika kabla ya kuwahi kufunga hizo siku sita, basi thawabu zake zinapotea isipokuwa kama amechelewesha kwa udhuru. Mtu akijaaliwa kufunga siku sita hizo kila jumatatu na alkhamisi basi analipwa thawabu mara mbili kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika kila kitendo kinategemea na nia na kila mmoja atalipwa kutokana na vile alivyonuia.”[1]
[1] al-Bukhaariy (1) na Muslim (1907).
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (20/18-19)
Imechapishwa: 06/06/2019
https://firqatunnajia.com/funga-shawwaal-jumatatu-na-alkhamisi-ulipwe-mara-mbili/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)