Swali: Je, kuna fadhilah yoyote ya kufunga siku sita za Shawwaal? Mtu afunge kwa kufululiza au kwa kuachanisha?
Jibu: Ndio, fadhilah zipo. Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayefunga Ramadhaan kisha akaifuatishia siku sita za Shawwaal basi ni kama ambaye amefunga mwaka mzima.”[1]
Mtu anatakiwa azingatie kwamba fadhilah hii haipatikani isipokuwa mpaka kwanza amalize kufunga Ramadhaan yote. Kwa ajili hiyo mtu akiwa na deni la Ramadhaan basi anatakiwa kulifunga kwanza kisha ndio afunge siku sita za Shawwaal. Vinginevyo mtu hapati thawabu hizi, ni mamoja swawm imesihi au haikusihi. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayefunga Ramadhaan kisha akaifuatishia… “
Yule mwenye deni la Ramadhaan kunasemwa kuwa amefunga baadhi ya Ramadhaan na haisemwi kuwa amefunga Ramadhaan.
Siku hizi sita inafaa zikawa zenye kufuatana au zenye kuachana. Lakini hata hivyo kuzifululiza ndio bora zaidi, kwanza ni kuharakisha kufanya matendo ya kheri, jengine mtu anaepuka mambo ya kuchelewa ambayo yanaweza kupelekea mtu asikamilishe funga.
[1] Muslim (1164).
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (20/17-18)
- Imechapishwa: 06/06/2019
Swali: Je, kuna fadhilah yoyote ya kufunga siku sita za Shawwaal? Mtu afunge kwa kufululiza au kwa kuachanisha?
Jibu: Ndio, fadhilah zipo. Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayefunga Ramadhaan kisha akaifuatishia siku sita za Shawwaal basi ni kama ambaye amefunga mwaka mzima.”[1]
Mtu anatakiwa azingatie kwamba fadhilah hii haipatikani isipokuwa mpaka kwanza amalize kufunga Ramadhaan yote. Kwa ajili hiyo mtu akiwa na deni la Ramadhaan basi anatakiwa kulifunga kwanza kisha ndio afunge siku sita za Shawwaal. Vinginevyo mtu hapati thawabu hizi, ni mamoja swawm imesihi au haikusihi. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayefunga Ramadhaan kisha akaifuatishia… “
Yule mwenye deni la Ramadhaan kunasemwa kuwa amefunga baadhi ya Ramadhaan na haisemwi kuwa amefunga Ramadhaan.
Siku hizi sita inafaa zikawa zenye kufuatana au zenye kuachana. Lakini hata hivyo kuzifululiza ndio bora zaidi, kwanza ni kuharakisha kufanya matendo ya kheri, jengine mtu anaepuka mambo ya kuchelewa ambayo yanaweza kupelekea mtu asikamilishe funga.
[1] Muslim (1164).
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (20/17-18)
Imechapishwa: 06/06/2019
https://firqatunnajia.com/hapa-ndipo-mtu-atapata-fadhilah-za-siku-sita-za-shawwaal/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)