Swali: Kipindi ambapo nilikuwa na miaka kumi baba yangu alisimama kutaka kunipiga kwa ajili ya jambo fulani na nikaanguka chini. Nikamuombea du´aa mbaya. Matokeo yake akanifukuza na akanipiga. Hivi sasa nina miaka thelathini na baba yangu ameshafariki.

Jibu: Ni lazima kwako kutubu kwa Allaah. Muda wa kuwa ulikuwa bado mdogo kipindi ambacho ´ibaadah haijakuwajibikia hakuna neno juu yako – Allaah akitaka. Lakini mwombee du´aa kwa wingi, msamaha na rehema kama mfano kusema:

اللهم ارحمه، اللهم اجزه عني خيرًا

“Ee Allaah, mrehemu! Ee Allaah, mlipe kheri kupitia kwangu!”

Kipindi hicho ulikuwa huna dhambi kwa njia ya kwamba ´ibaadah zilikuwa hazijakuwajibikia. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Kalamu imenyanyuliwa kwa watu watatu; aliyelala hadi aamke, mdogo hadi abaleghe na mwendawazimu hadi apate fahamu.”

Wewe kipindi hicho ´ibaadah zilikuwa bazo hazijakuwabikia. Namuomba Allaah akusamehe. Lakini hata hivyo mwombee du´aa kwa wingi.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa-ud-Duruus https://binbaz.org.sa/fatwas/4613/%D8%A8%D9%85-%D9%8A%D9%86%D8%B5%D8%AD-%D9%85%D9%86-%D8%B9%D9%82-%D9%88%D8%A7%D9%84%D8%AF%D9%87-%D8%B9%D9%86%D8%AF%D9%85%D8%A7-%D9%83%D8%A7%D9%86-%D8%B5%D8%BA%D9%8A%D8%B1%D8%A7
  • Imechapishwa: 24/09/2020