Alikuwa akidhani kuwa swalah sio faradhi

Swali: Baba yangu amekufa miaka kumi iliyopita. Alikuwa anajinasibisha na Uislamu lakini hata hivyo alikuwa haswali kwa sababu alikuwa anadhani kuwa swalah imependekezwa tu na sio faradhi. Je, nimuombee msamaha?

Jibu: Kwa kweli sijihisi sawa nafsini kumuombea du´aa na msamaha mtu ambaye haswali. Kwa sababu hana dini. Lakini ikiwa kweli alikuwa hajui, kama jinsi ulivosema, basi anazingatiwa ni miongoni mwa watu ambao hawakufikiwa na Mtume.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (89) https://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/%D8%A5%D8%BA%D8%A7%D8%AB%D8%A9%20%D8%A7%D9%84%D9%84%D9%87%D9%81%D8%A7%D9%86%20%D9%85%D9%86%20%D9%85%D8%B5%D8%A7%D9%8A%D8%AF%20%D8%A7%D9%84%D8%B4%D9%8A%D8%B7%D8%A7%D9%86-08-07-1439.lite__0.mp3