Kuwepo juu kwa Allaah ni katika sifa ambazo Ahl-us-Sunnah wamezozana sana na wale wenye kwenda kinyume miongoni mwa Ahl-ul-Bid´ah. Ni miongoni mwa sifa kuu ambazo wanafalsafa na Ahl-ul-Bid´ah wamezikanusha.

Tumetangulia kusema kwamba kuna sifa tatu yule mwenye kuzithibitisha basi tambueni kuwa ni katika Ahl-us-Sunnah na mwenye kuzipinga basi tambueni vilevile kuwa ni katika Ahl-ul-Bid´ah. Nazo ni hizi zifuatazo:

1- Maneno [kuzungumza kwa Allaah].

2- Kuonekana kwa Allaah Aakhirah.

3- Allaah kuwa juu.

Sifa hizi tatu ndio alama yenye kupambanua baina ya Ahl-us-Sunnah na Ahl-ul-Bid´ah. Miongoni mwa waliozikanusha ni Ashaa´irah na Jahmiyyah. Watu hawa wamekanusha kuwepo juu kwa Allaah na Maneno. Maneno kwa mujibu wa Ashaa´irah ni kitu kilichosimama katika nafsi. Lakini wakathibitisha kuonekana kwa Allaah Aakhirah. Kwa vile ni miongoni mwa watu wenye kukanusha kuwa Allaah Yuko juu ndio wakasema kuwa ataonekana lakini si katika upande hata mmoja. Hivyo wenye busara wakawazomea.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajhiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Hidaayah ar-Rabbaaniyyah fiy Sharh al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah (01/401)
  • Imechapishwa: 19/05/2020