Swali: Je, imepokelewa kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alihimiza adhaana ya kwanza kwa ajili ya Fajr? Kuna muda kiasi gani kati ya adhaana ya kwanza na adhaana ya pili?
Jibu: Adhaana ya kwanza imependekezwa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Bilaal anaadhini usiku. Hivyo kuleni na kunyweni mpaka aadhini Ibn Umm Maktuum.”
Mpokezi amesema:
“Alikuwa ni mtu kipofu na haadhini mpaka aambiwe “kumepambazuka, kumepambazuka.”
Hii inafahamisha kwamba yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimkubalia Bilaal kitendo chake na (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akabainisha hekima ya hilo kwa kusema katika moja ya mapokezi:
“Bilaal anaadhini usiku ili kumuamsha aliyelala katika nyinyi na kumrejesha aliye macho katika nyinyi… “
Katika kufanya hivo hakuna kikomo maalum. Bora adhaana ya kwanza iwe karibu na adhaana ya mwisho. Hayo ni kutokana na maneno ya mpokezi katika baadhi ya mapokezi:
“Hakukuwa kati yazo isipokuwa kitambo cha kupanda huyu na kushuka mwengine.”
Kwa msemo mwingine ni kwamba hakukuwa kazi yazo isipokuwa kitambo kifupi.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (10/341)
- Imechapishwa: 19/09/2021
Swali: Je, imepokelewa kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alihimiza adhaana ya kwanza kwa ajili ya Fajr? Kuna muda kiasi gani kati ya adhaana ya kwanza na adhaana ya pili?
Jibu: Adhaana ya kwanza imependekezwa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Bilaal anaadhini usiku. Hivyo kuleni na kunyweni mpaka aadhini Ibn Umm Maktuum.”
Mpokezi amesema:
“Alikuwa ni mtu kipofu na haadhini mpaka aambiwe “kumepambazuka, kumepambazuka.”
Hii inafahamisha kwamba yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimkubalia Bilaal kitendo chake na (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akabainisha hekima ya hilo kwa kusema katika moja ya mapokezi:
“Bilaal anaadhini usiku ili kumuamsha aliyelala katika nyinyi na kumrejesha aliye macho katika nyinyi… “
Katika kufanya hivo hakuna kikomo maalum. Bora adhaana ya kwanza iwe karibu na adhaana ya mwisho. Hayo ni kutokana na maneno ya mpokezi katika baadhi ya mapokezi:
“Hakukuwa kati yazo isipokuwa kitambo cha kupanda huyu na kushuka mwengine.”
Kwa msemo mwingine ni kwamba hakukuwa kazi yazo isipokuwa kitambo kifupi.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (10/341)
Imechapishwa: 19/09/2021
https://firqatunnajia.com/adhaana-ya-kwanza-katika-swalah-ya-fajr-imependekezwa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)