4 – Miongoni mwa sababu za kuhifadhi tupu ni kukataza faragha kati ya mwanamke na mwanaume ambaye sio Mahram yake. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yule ambaye anamwamini Allaah na siku ya Mwisho basi asikae faragha na mwanamke ambaye hana Mahram yake – kwani watatu wao ni shaytwaan.”
´Aamir bin Rabiy´ah amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwanamume asikae faragha na mwanamke ambaye si halali kwake. Kwani hakika watatu wao ni shaytwaan; isipokuwa Mahram.”
al-Majid amesema katika “al-Muntaqaa´”:
“Ameipoikea Ahmad na imekwishatangulia maana yake kwa Ibn ´Abbaas katika Hadiyth iliopokelewa na al-Bukhaariy na Muslim.”
Imaam ash-Shawkaaniy amesema katika “Nayl-ul-Awtwaar”:
“Kuna maafikiano juu ya kwamba ni haramu kukaa faragha na ambaye ni ajinabi, hayo yamesimuliwa na Haafidhw katika “al-Fath”. Sababu ya uharamu ni ile iliyotajwa katika Hadiyth kwamba watatu wao ni shaytwaan. Uwepo wake utawafanya kutumbukia katika madhambi. Ama kwa pamoja na kuwepo kwa Mahram kukaa faragha na ambaye ni ajinabi inafaa na kutowezekana kutokea madhambi pamoja na uwepo wake.”[1]
[1] (06/120).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 124
- Imechapishwa: 11/12/2019
4 – Miongoni mwa sababu za kuhifadhi tupu ni kukataza faragha kati ya mwanamke na mwanaume ambaye sio Mahram yake. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yule ambaye anamwamini Allaah na siku ya Mwisho basi asikae faragha na mwanamke ambaye hana Mahram yake – kwani watatu wao ni shaytwaan.”
´Aamir bin Rabiy´ah amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwanamume asikae faragha na mwanamke ambaye si halali kwake. Kwani hakika watatu wao ni shaytwaan; isipokuwa Mahram.”
al-Majid amesema katika “al-Muntaqaa´”:
“Ameipoikea Ahmad na imekwishatangulia maana yake kwa Ibn ´Abbaas katika Hadiyth iliopokelewa na al-Bukhaariy na Muslim.”
Imaam ash-Shawkaaniy amesema katika “Nayl-ul-Awtwaar”:
“Kuna maafikiano juu ya kwamba ni haramu kukaa faragha na ambaye ni ajinabi, hayo yamesimuliwa na Haafidhw katika “al-Fath”. Sababu ya uharamu ni ile iliyotajwa katika Hadiyth kwamba watatu wao ni shaytwaan. Uwepo wake utawafanya kutumbukia katika madhambi. Ama kwa pamoja na kuwepo kwa Mahram kukaa faragha na ambaye ni ajinabi inafaa na kutowezekana kutokea madhambi pamoja na uwepo wake.”[1]
[1] (06/120).
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 124
Imechapishwa: 11/12/2019
https://firqatunnajia.com/71-sababu-ya-tatu-ya-kuhifadhi-tupu-kukaa-faragha-mwanamume-na-mwanamke/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)