Abu Muhammad ´Abdullaah bin Abiy Zayd al-Qayrawaaniy (Rahimahu Allaah) amesema:
Alijionyesha mlimani ambapo ukapasukapasuka kutokana na utukufu Wake.
MAELEZO
Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
فَلَمَّا تَجَلَّىٰ رَبُّهُ لِلْجَبَلِ جَعَلَهُ دَكًّا
“Basi Mola wako alipojidhihirisha katika mlima akalifanya livurugike kuwa vumbi.”
Wakati Muusa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliposikia maneno ya Mola wake, ndipo akatamani pia kumuona na akasema:
رَبِّ أَرِنِي أَنظُرْ إِلَيْكَ
“Mola wangu! Nionyeshe ili nikutazame.”[1]
Allaah akamjibu:
لَن تَرَانِي وَلَـٰكِنِ انظُرْ إِلَى الْجَبَلِ فَإِنِ اسْتَقَرَّ مَكَانَهُ فَسَوْفَ تَرَانِي
“(Lan) Hutoniona! Lakini tazama jabali. Likitulia mahali pake, basi utaniona.”[2]
Huna uwezo wa kuniona. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) akataka kumbainishia hilo kwa kumuonyesha ni kipi kitachoutokea mlima ikiwa atajionyesha:
وَلَـٰكِنِ انظُرْ إِلَى الْجَبَلِ فَإِنِ اسْتَقَرَّ مَكَانَهُ فَسَوْفَ تَرَانِي
”… lakini tazama jabali. Likitulia mahali pake, basi utaniona.”[3]
Mlima ulipasukapasuka na kuwa changarawe.
وَخَرَّ مُوسَىٰ صَعِقًا
“… na Muusa akaanguka hali ya kuzimia.”[4]
Kwa sababu ya woga.
[1] 7:143
[2] 7:143
[3] 7:143
[4] 7:143
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Bayaan-ul-Ma´aaniy fiy Sharh Muqaddimati Ibn Abiy Zayd al-Qayrawaaniy, uk. 41-42
- Imechapishwa: 02/08/2021
Abu Muhammad ´Abdullaah bin Abiy Zayd al-Qayrawaaniy (Rahimahu Allaah) amesema:
Alijionyesha mlimani ambapo ukapasukapasuka kutokana na utukufu Wake.
MAELEZO
Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
فَلَمَّا تَجَلَّىٰ رَبُّهُ لِلْجَبَلِ جَعَلَهُ دَكًّا
“Basi Mola wako alipojidhihirisha katika mlima akalifanya livurugike kuwa vumbi.”
Wakati Muusa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliposikia maneno ya Mola wake, ndipo akatamani pia kumuona na akasema:
رَبِّ أَرِنِي أَنظُرْ إِلَيْكَ
“Mola wangu! Nionyeshe ili nikutazame.”[1]
Allaah akamjibu:
لَن تَرَانِي وَلَـٰكِنِ انظُرْ إِلَى الْجَبَلِ فَإِنِ اسْتَقَرَّ مَكَانَهُ فَسَوْفَ تَرَانِي
“(Lan) Hutoniona! Lakini tazama jabali. Likitulia mahali pake, basi utaniona.”[2]
Huna uwezo wa kuniona. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) akataka kumbainishia hilo kwa kumuonyesha ni kipi kitachoutokea mlima ikiwa atajionyesha:
وَلَـٰكِنِ انظُرْ إِلَى الْجَبَلِ فَإِنِ اسْتَقَرَّ مَكَانَهُ فَسَوْفَ تَرَانِي
”… lakini tazama jabali. Likitulia mahali pake, basi utaniona.”[3]
Mlima ulipasukapasuka na kuwa changarawe.
وَخَرَّ مُوسَىٰ صَعِقًا
“… na Muusa akaanguka hali ya kuzimia.”[4]
Kwa sababu ya woga.
[1] 7:143
[2] 7:143
[3] 7:143
[4] 7:143
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Bayaan-ul-Ma´aaniy fiy Sharh Muqaddimati Ibn Abiy Zayd al-Qayrawaaniy, uk. 41-42
Imechapishwa: 02/08/2021
https://firqatunnajia.com/51-allaah-alijidhihirisha-kwenye-mlima/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)