5. Ni wajibu kufuata Qur-aan peke yake

Allaah (Ta´ala) amesema:

وَنَزَّلْنَا عَلَيْكَ الْكِتَابَ تِبْيَانًا لِّكُلِّ شَيْءٍ

“Na Tumekuteremshia Kitabu hali ya kuwa ni chenye kubainisha kila kitu.” (16:89)

an-Nasaa´iy na wengine wamepokea ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliona mikononi mwa ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) karatasi ya Tawraat akasema:

“Ee mwana wa al-Khattwaab! Una shaka? Nimekufikishieni waziwazi kabisa. Lau Muusa angelikuwa hai hii leo mkamfuata badala ya kunifuata mimi basi mgelikuwa mmepotea.” Ndipo ´Umar akasema: “Nimeridhia Allaah kuwa Mola Wangu, Uislamu kuwa dini yangu na Muhammad kuwa Mtume wangu.”[1]

Katika upokezi mwingine imekuja:

“Lau Muusa angelikuwa hai hii leo asingelikuwa na namna isipokuwa kunifuata.”

[1] Ahmad (3/387), ad-Daarimiy (436), Abu Ya´laa (4/102) na wengineo.

  • Mhusika: Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fadhwl-ul-Islaam, uk. 18
  • Imechapishwa: 23/10/2016