Swali 40: Swali: Ni ipi hukumu ya swalah ya ijumaa ikikumbana na siku ya ´iyd? Je, itakuwa ni lazima kwa waislamu wote kuiswali au kikosi maalum? Wako watu wanaoamini kwamba ´iyd ikikutana na ijumaa basi hapo hakuna ijumaa[1].
Jibu: Ni lazima kwa imamu na khatwiyb waswalishe ijumaa na wahudhurie msikitini kuwaswalisha wale watakaohudhuria. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiswali ´iyd na ijumaa. Wakati mwingine akisoma katika ´iyd na ijumaa Suurah “al-A´laa” na “al-Ghaashiyah” katika swalah zote hizo mbili. Hayo yamesemwa na an-Nu´maan bin Bashiyr (Radhiya Allaahu ´anh) kama ilivyothibiti katika “as-Swahiyh”.
Lakini yule mtu ambaye atahudhuria ´iyd inafaa kwake kuacha kuswali ijumaa na badala yake ataswali Dhuhr nyumbani kwake au pamoja na baadhi ya ndugu zake akiwa alihudhuria swalah ya ´iyd. Endapo ataswali ijumaa pamoja na wengine ndio bora na kamilifu zaidi. Na akiacha kuswali swalah ya ijumaa kwa sababu alihudhuria na kuswali ´iyd ni sawa kwake. Lakini ni lazima kwake kuiswali kwa aina ya Dhuhr. Ni mamoja atafanya hivo peke yake au na wengine.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (12/341-342).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahkaam Swalaat-il-Jumu´ah wal-Jamaa´ah, uk. 79-80
- Imechapishwa: 04/12/2021
Swali 40: Swali: Ni ipi hukumu ya swalah ya ijumaa ikikumbana na siku ya ´iyd? Je, itakuwa ni lazima kwa waislamu wote kuiswali au kikosi maalum? Wako watu wanaoamini kwamba ´iyd ikikutana na ijumaa basi hapo hakuna ijumaa[1].
Jibu: Ni lazima kwa imamu na khatwiyb waswalishe ijumaa na wahudhurie msikitini kuwaswalisha wale watakaohudhuria. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiswali ´iyd na ijumaa. Wakati mwingine akisoma katika ´iyd na ijumaa Suurah “al-A´laa” na “al-Ghaashiyah” katika swalah zote hizo mbili. Hayo yamesemwa na an-Nu´maan bin Bashiyr (Radhiya Allaahu ´anh) kama ilivyothibiti katika “as-Swahiyh”.
Lakini yule mtu ambaye atahudhuria ´iyd inafaa kwake kuacha kuswali ijumaa na badala yake ataswali Dhuhr nyumbani kwake au pamoja na baadhi ya ndugu zake akiwa alihudhuria swalah ya ´iyd. Endapo ataswali ijumaa pamoja na wengine ndio bora na kamilifu zaidi. Na akiacha kuswali swalah ya ijumaa kwa sababu alihudhuria na kuswali ´iyd ni sawa kwake. Lakini ni lazima kwake kuiswali kwa aina ya Dhuhr. Ni mamoja atafanya hivo peke yake au na wengine.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (12/341-342).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ahkaam Swalaat-il-Jumu´ah wal-Jamaa´ah, uk. 79-80
Imechapishwa: 04/12/2021
https://firqatunnajia.com/40-kuswali-ijumaa-siku-ya-iyd/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)