36- Muhammad ametukhabarisha: Ahmad ametuhadithia: Haafidhw Abu Nu´aym ametuhadithia: Abu Bakr bin Khallaad ametuhadithia: al-Haarith bin Abiy Usaamah ametuhadithia: Abu Nu´aym ametuhadithia: al-A´mash ametuhadithia, kutoka kwa Ibraahiym at-Taymiy, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Abu Dharr (Radhiya Allâhu ´anh) ambaye amesema:
“Tulikuwa tumeketi kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) msikitini wakati jua lilipozama. Akasema: “Ee Abu Dharr! Je, unajua ni wapi jua linapozamia?”Nikajibu: “Allaah na Mtume wake ndio wajuzi zaidi.” Akasema: “Linaenda mpaka linasujudu chini ya ´Arshi kwa Mola wake na linaomba idhini. Linaomba idhini na halipewi idhini mpaka lishufai na kutaka. Baada ya muda mrefu ndio huambiwa: “Chomoza sehemu yako.” Hiyo ndio tafsiri ya maneno Yake (Ta´ala):
وَالشَّمْسُ تَجْرِي لِمُسْتَقَرٍّ لَّهَا ۚ ذَٰلِكَ تَقْدِيرُ الْعَزِيزِ الْعَلِيمِ
“Jua linatembea hadi matulio yake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu kabisa, Mjuzi wa yote.”[1][2]
[1] 36:38
[2] al-Bukhaariy (3199) na Muslim (159).
- Mhusika: Imaam Muwaffaq-ud-Diyn bin Qudaamah al-Maqdisiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ithbaatu Swifat-il-´Uluww, uk. 129-130
- Imechapishwa: 18/06/2018
36- Muhammad ametukhabarisha: Ahmad ametuhadithia: Haafidhw Abu Nu´aym ametuhadithia: Abu Bakr bin Khallaad ametuhadithia: al-Haarith bin Abiy Usaamah ametuhadithia: Abu Nu´aym ametuhadithia: al-A´mash ametuhadithia, kutoka kwa Ibraahiym at-Taymiy, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Abu Dharr (Radhiya Allâhu ´anh) ambaye amesema:
“Tulikuwa tumeketi kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) msikitini wakati jua lilipozama. Akasema: “Ee Abu Dharr! Je, unajua ni wapi jua linapozamia?”Nikajibu: “Allaah na Mtume wake ndio wajuzi zaidi.” Akasema: “Linaenda mpaka linasujudu chini ya ´Arshi kwa Mola wake na linaomba idhini. Linaomba idhini na halipewi idhini mpaka lishufai na kutaka. Baada ya muda mrefu ndio huambiwa: “Chomoza sehemu yako.” Hiyo ndio tafsiri ya maneno Yake (Ta´ala):
وَالشَّمْسُ تَجْرِي لِمُسْتَقَرٍّ لَّهَا ۚ ذَٰلِكَ تَقْدِيرُ الْعَزِيزِ الْعَلِيمِ
“Jua linatembea hadi matulio yake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu kabisa, Mjuzi wa yote.”[1][2]
[1] 36:38
[2] al-Bukhaariy (3199) na Muslim (159).
Mhusika: Imaam Muwaffaq-ud-Diyn bin Qudaamah al-Maqdisiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ithbaatu Swifat-il-´Uluww, uk. 129-130
Imechapishwa: 18/06/2018
https://firqatunnajia.com/38-dalili-ya-thelathini-na-sita-kutoka-katika-sunnah-kwamba-allaah-yuko-juu-ya-viumbe/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)