21. Hakuna tofauti kati ya al-Albaaniy na wanachuoni wa Saudia

Ninavyoamini ni kwamba Salafiyyah alionayo al-Albaaniy ndio Salafiyyah ileile walionayo wanachuoni wa Saudi Arabia kama mfano wa Shaykh ´Abdul-´Aziyz bin Baaz, Ibn ´Uthaymiyn, al-Fawzaan, ´Abdul-´Aziyz Aalush-Shaykh na wengineo. Anaamini yale wanayoamini juu ya majina na sifa za Allaah, Qadar, kwamba Qur-aan ni maneno ya Allaah yaliyoteremshwa na haikuumbwa na I´tiqaad nyenginezo. Kama kuna tofauti ndogo basi ni katika mambo ya Ijtihaad. Ama katika ´Aqiydah, hakuna tofauti kati yake yeye na wao.

  • Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Fath ar-Rabbaaniy fiyd-Difaa´ ´an-ish-Shaykh Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy, uk. 44
  • Imechapishwa: 03/12/2018