Zihifadhini sifa za Khawaarij ili mtahadhari nao!

Hizi ndio sifa zao – Khawaarij – zihifadhini:

1- Wadogo kiumri.

2- Wapumbavu wa akili.

3- Wanazungumza kwa maneno matamu kabisa.

4- Wanatoka katika Dini kama jinsi mshale unavotoka kwenye upinde wake.

5- Anayekutana nao awaue – hii ndio hukumu yao – kwa kuwa katika kuwaua kuna ujira mbele ya Allaah.

Ni wadogo kiumri. Vijana wasiotaka kusikia maneno wala kurejea kwa wanachuoni. Mienendo yao ni kama hii na wanawadharua wanachuoni na wanasema kuwa ni wanachuoni wa hedhi na nifasi na maneno mengine ambayo wanawasifu wanachuoni. Ni wadogo kiumri na kati yao hakuna mtu aliyeoongoka na wote vilevile ni wapumbavu wa akili. Katika wao hakuna mtu mwenye akili na mwongofu. Wote hizi ndio sifa zao na hatoki katika sifa hizi yeyote. Huu ndio uhakika wao katika kila zama na sio katika zama moja tu. Hawatoacha kutoka wakiwa namna hii mpaka atapotokea ad-Dajjaal. Kila kinapokatika kizazi chao kunajitokeza kingine. Wako na sifa hizi. Wanadharau elimu na wanachuoni na mfumo wa Qur-aan na Sunnah na kadhalika. Wanaufanyia Ummah Takfiyr na watawala. Wanaonelea kujuzu kuwafanyia uasi, wanawaua [wasiostahiki kuuawa], wanawasha fitina na wanamwaga damu na tunaomba kinga kwa Allaah.

Kwa ajili hii ndio maana ´Aliy aliwapiga vita watu hawa na akabainisha ujira kwa mwenye kuwaua.

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: adh-Dhariy´ah ilaa Bayaan Maqaasid Kitaab-ish-Sharï´ah (1/151)
  • Imechapishwa: 19/05/2015