Swali 305: Vipi wakati mtu anamuitikia muadhini kusema:
إنك لا تخلف الميعاد
“Hakika wewe hauendi kinyume na ahadi Yako”?
Jibu: Hadiyth hii ya Zayd ndani yake kuna ziada mbili na zote mbili ni dhaifu. Moja ni isemayo:
اللهم رب هذه الدعوة التامة، والصلاة القائمة، آت سيدنا محمد الوسيلة والفضيلة
“Ee Allaah, Mola wa mwito huu uliotimia, swalah iliosimama, mpe bwana wetu Muhammad, Wasiylah na fadhilah… “
Tamko la:
سيدنا محمد
“Bwana wetu Muhammad”
linazingatiwa kuwa ni dhaifu. Aliliongeza at-Twahaawiyyah katika “Sharh al-Maa´niy al-Aathaar”. Linazingatiwa kuwa ni dhaifu. Ziada ya pili pia inazingatiwa kuwa ni dhaifu. Linasema:
إنك لا تخلف الميعاد
“Hakika wewe huendi kinyume na ahadi Yako.”
Muhammad bin ´Awf at-Twaai’ amepwekeka nayo. Wengi wamekwenda kinyume naye. Kwa hiyo tamko hilo linazingatiwa ni dhaifu kama nilivyoyataja hayo katika “ash-Shafaa´ah”. Muhammad bin ´Awf at-Twaai’ amepwekeka nayo. Imaam al-Bayhaqiy ameipokea katika “as-Sunan”. Kwa hiyo ziada mbili hizi ni dhaifu.
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ijaabatu as-Saa-il, uk. 549
- Imechapishwa: 23/02/2020
Swali 305: Vipi wakati mtu anamuitikia muadhini kusema:
إنك لا تخلف الميعاد
“Hakika wewe hauendi kinyume na ahadi Yako”?
Jibu: Hadiyth hii ya Zayd ndani yake kuna ziada mbili na zote mbili ni dhaifu. Moja ni isemayo:
اللهم رب هذه الدعوة التامة، والصلاة القائمة، آت سيدنا محمد الوسيلة والفضيلة
“Ee Allaah, Mola wa mwito huu uliotimia, swalah iliosimama, mpe bwana wetu Muhammad, Wasiylah na fadhilah… “
Tamko la:
سيدنا محمد
“Bwana wetu Muhammad”
linazingatiwa kuwa ni dhaifu. Aliliongeza at-Twahaawiyyah katika “Sharh al-Maa´niy al-Aathaar”. Linazingatiwa kuwa ni dhaifu. Ziada ya pili pia inazingatiwa kuwa ni dhaifu. Linasema:
إنك لا تخلف الميعاد
“Hakika wewe huendi kinyume na ahadi Yako.”
Muhammad bin ´Awf at-Twaai’ amepwekeka nayo. Wengi wamekwenda kinyume naye. Kwa hiyo tamko hilo linazingatiwa ni dhaifu kama nilivyoyataja hayo katika “ash-Shafaa´ah”. Muhammad bin ´Awf at-Twaai’ amepwekeka nayo. Imaam al-Bayhaqiy ameipokea katika “as-Sunan”. Kwa hiyo ziada mbili hizi ni dhaifu.
Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ijaabatu as-Saa-il, uk. 549
Imechapishwa: 23/02/2020
https://firqatunnajia.com/ziada-mbili-dhaifu-katika-adhaana/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)