Zakaah juu ya pesa ya kodi anayopokea mwenye nyumba

Swali: Nina mali isiyohamishika (nyumba/ardhi) niliyoipangisha kwa kiasi cha 18,000 kwa mwaka. Nilipokea nusu ya kiasi hicho mapema na iliyobaki mwisho wa mwaka. Ninatumia sehemu yake kuwalisha watoto wangu. Je, inanilazimu kutoa zakaah?

Jibu: Ikiwa mapato ya kodi yatazungukiwa na mwaka, basi ni wajibu kuitolea zakaah. Ikiwa atapokea kisha akaitumia kabla ya kukamilika mwaka wake, akazitumia katika mahitaji yake, basi hakuna zakaah juu yake. Lakini ikiwa mwaka umepita juu ya mapato yote au juu ya sehemu yake, basi atatoa zakaah ya kiasi kilichopitiwa na mwaka.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1392/حكم-زكاة-اجرة-العقار-وبيان-وقت-اخراجها
  • Imechapishwa: 13/12/2025