Ya´juuj na Ma´juuj ni wachina? ukuta wa kinga ni wa kichina?

Swali: Je, ni sahihi kuwa Ya´juuj na Ma´juuj ni wachina na ukuta wa kinga ni ule ukuta wa kichina?

Jibu: Ni nani mwenye kusema hivi? Hakuna mwenye elimu anayesema hivo. Wajinga tu au wadau ndio wenye kusema hivi. Allah ndiye Anajua zaidi. Nyinyi mmeitembea ardhi yote na hamkuacha kitu kilichofichikana kwenu? Hakuna yeyote amefanya hivo. Hata wale wenye uwezo. Hawakufichua mambo yote. Bado kuna mambo hawayajui.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Muqaddimati Ibn Abiy Zayd al-Qayrawaaniy fiyl-´Aqiydah (05) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/qir–14340106.mp3
  • Imechapishwa: 17/06/2015