Swali: Kuna mwalimu aliwaambia wanafunzi wake maneno yafuatayo:
“Allaah amelingana juu ya ´Arshi Yake pasi na kuigusa halafu akajirudi.”
Akasema tena:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikosea katika kisa aliyekunja kipaji na akageuka kisha akajirudi.”
Akasema tena:
“Amemmnasibishia Shaykh-ul-Islaam [Ibn Taymiyyah] maoni ya Tasalsul kisha akajirudi.”
Vivyo hivyo ana makosa mengi ambayo anajirudi hapa na hapa. Je, mtu asome kwa Shaykh kama huyu?
Jibu: Huyu ni mwenye mashaka. Huyu anawatia watu mashaka katika mambo ya ´Aqiydah yao. Haijuzu kusoma kwake wala kuchukua elimu kutoka kwake. Kwa kuwa huyu ni katika wapotevu. Anawatia watu mashaka na anadhihrisha ´Aqiydah yake batili. Pale anapoona watu wanamkemea ndipo anajifanya kuwa anajirudi kihadaa. Haijuzu kumkubalia mtu huyu wala kusoma kwake. Bali ni wajibu kutahadhari naye.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://www.youtube.com/watch?v=Snc73LjWfPE&feature=youtu.be
- Imechapishwa: 26/10/2016
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)