Imesemekana kuwa Ibn ´Atwaa´ alipoteza akili yake akiwa na miaka kumi na nane kisha baadaye akili yake ikamrudi. Tunamuomba Allaah aifanye imara akili na imani yetu. Yule mwenye kusababisha kupoteza akili yake kwa njaa, mazoezi magumu na kuipa nyongo dunia basi ameasi na kutenda dhambi. Amefanana na yule ambaye ameipoteza akili yake kwa kutumia kilevi. Ni uzuri uliyoje wa kushikamana na Sunnah na elimu!

  • Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (14/256)
  • Imechapishwa: 03/11/2020