Swali 340: Akiwepo kijana anayetaka kutafuta elimu na wazazi wake wanamkataza na wanachotaka ni yeye aende katika Jihaad. Je, awatii katika jambo hilo?
Jibu: Apambane na wao. Haijuzu kwake kwenda ilihali wazazi wake wanamkataza. Kuhusu kujifunza elimu ambayo Allaah amemuwajibishia basi:
“Hakika hakuna utiifu kwa kiumbe katika kumuasi Muumba.”
Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) kama ilivyo katika “al-Masaa-il” ya Ibn Haaniy (Rahimahu Allaah) ambaye amesimulia: “Kuna mtu alimuuliza Imaam Ahmad kuhusu mtu ambaye amekatazwa na baba yake, mama yake au wazazi wake kutafuta elimu akajibu:
“Asiwatii.”
Hilo ni tofauti na Jihaad. Vivyo hivyo iwapo mama yake atamkataza swalah ya mkusanyiko asimtii. al-Hasan al-Baswriy (Rahimahu Allaah) alisema hivo.
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ijaabatu as-Saa-il, uk. 582
- Imechapishwa: 07/12/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket