Swali: Je, inajuzu kwa mwanamke kujizuia kuolewa baada ya kufiliwa na mume wake wa kwanza au mwanamume akamuamrisha mke wake asiolewe na mwanaume mwingine endapo yeye atakufa kabla yake?
Jibu: Haijuzu kwa mwanamke kujizuia kuolewa baada ya kufiliwa na mume wake. Hayo ni mambo maalum kwa wakeze Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) peke yake.
Vilevile haijuzu kwa mwanaume kumkataza mke wake kuolewa baada ya yeye kufa na wala haimlazimu mwanamke kumtii katika hilo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika utiifu unakuwa katika mambo mema.”[1]
[1] al-Bukhaariy (7145), Muslim (1840), an-Nasaa´iy (4205) na wengineo.
- Muhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (18/18)
- Imechapishwa: 04/08/2017
Swali: Je, inajuzu kwa mwanamke kujizuia kuolewa baada ya kufiliwa na mume wake wa kwanza au mwanamume akamuamrisha mke wake asiolewe na mwanaume mwingine endapo yeye atakufa kabla yake?
Jibu: Haijuzu kwa mwanamke kujizuia kuolewa baada ya kufiliwa na mume wake. Hayo ni mambo maalum kwa wakeze Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) peke yake.
Vilevile haijuzu kwa mwanaume kumkataza mke wake kuolewa baada ya yeye kufa na wala haimlazimu mwanamke kumtii katika hilo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika utiifu unakuwa katika mambo mema.”[1]
[1] al-Bukhaariy (7145), Muslim (1840), an-Nasaa´iy (4205) na wengineo.
Muhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (18/18)
Imechapishwa: 04/08/2017
https://firqatunnajia.com/waume-wanaowakataza-wake-zao-kuolewa-baada-ya-kufa/