Suala kuhusiana na wingi wa makundi linahitajia kuandikwa katika kitabu ili wapate kujua ya kuwa watu wanaoruhusu [uwepo wa] makundi mengi kama Yuusuf al-Qaradhwaawiy, ‘Abdul-Wahhaab ad-Daylamiy, Swalaah as-Saawiy na ‘Aqiyl al-Matrafiy wanaita katika machafuko. Ni lazima kuwepo wanafunzi ambao watachukua [jukumu hili] la kuandika kitabu kilico na Hadiyth na Aayah za Qur-aan ili kufichukua hali za watu hawa.

Swalaah as-Saawiy ndio mrithi wa wa Sa’iyd Hawwaa. Wewe, Swalaah as-Saawiy, utakufa kama jinsi vitabu vyako na fikira zako zitavyokufa. Vivyo hivyo ndivyo alivyokufa Sa’iyd Hawwaa, vitabu vyake na fikira zake. Najua ya kuwa ulikuwa mtu mwema wakati ulipokuja Misri. Ninakutahadharisha kufa katika hali hii. Unaita katika tofauti na mgawanyiko kati ya Waislamu na kutekeleza kampeni za Marekani. Marekani inataka tubaki hali ya kuwa ni wenye tofauti na tumegawanyika.

  • Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fadhwaaih wa Naswaaih, uk. 102
  • Imechapishwa: 19/04/2015