Waswaliji kila mmoja anaswali mita moja mbali na mwenzie kwa ajili ya kuepuka maambukizi

Swali: Kuna baadhi ya misikiti wanaswali na kati ya kila mswaliji kuna uwazi wa kiasi cha mita moja au mbili wakidai kwamba kufanya hivo ni kujizuia na maradhi [maambukizi ya corona]. Ni ipi hukumu ya hilo?

Jibu: Swalah haisihi. Wanazingatiwa ameswali mmoja mmoja kama ambavo anaswali mtu kivyake.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-Muhsin bin Hamad al-´Abbaad
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh al-Muwatta’ (19)
  • Imechapishwa: 07/04/2020