Zayd bin Khaalid al-Juhaniy (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
”Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alituswalisha Swalah ya Subh Hudaybiyah baada ya usiku ulionyesha. Wakati alipomaliza aliwageukia watu na kusema: ”Mnajua nini amesema Mola Wenu?” Wakasema: ”Allaah na Mtume Wake ndiyo wenye kujua zaidi.” Akasema: ”Baadhi ya waja wangu wameamka hali ya kuwa ni waumini na wengine makafiri. Waliosema: ”Tumenyeshelezewa kwa sababu ya fadhila na Rahmah za Allaah” wananiamini Mimi na wanakanusha nyota. Ama wale waliosema: ”Tumenyeshelezewa kwa sababu ya nyota kadhaa na kadhaa” anaamini nyota na amenikanusha Mimi.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Imesemekana kwamba kuomba du´aa wakati wa kunyesha mvua ni jambo lililopendekezwa.
´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
”Wakati Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipokuwa anaona mvua, husema:
اللّهُمَّ صَيِّـباً نافِـعاً
“Ee Allaah! Iteremshe kwa wingi na iwe yenye manufaa!”[2]
Anas (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Mvua ilinyesha nasi tukiwa pamoja na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam). Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) akakunja nguo yake ili mvua impate. Tukasema: ”Ee Mtume wa Allaah, kwa nini umefanya hivo?” Akasema: ”Kwa sababu ndio punde imetoka kwa Mola wake.” [3]
Ameipokea Muslim.
[1] al-Bukhaariy (846, 1037 na 4147) na Muslim (71).
[2] al-Bukhaariy (1032).
[3] Muslim (898).
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Abiy Bakr bin Qayyim-il-Jawziyyah (afk. 751)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Waabil as-Swayyib wa Raafi´-ul-Kalim at-Twayyib, uk. 320
- Imechapishwa: 09/09/2025
Zayd bin Khaalid al-Juhaniy (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
”Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alituswalisha Swalah ya Subh Hudaybiyah baada ya usiku ulionyesha. Wakati alipomaliza aliwageukia watu na kusema: ”Mnajua nini amesema Mola Wenu?” Wakasema: ”Allaah na Mtume Wake ndiyo wenye kujua zaidi.” Akasema: ”Baadhi ya waja wangu wameamka hali ya kuwa ni waumini na wengine makafiri. Waliosema: ”Tumenyeshelezewa kwa sababu ya fadhila na Rahmah za Allaah” wananiamini Mimi na wanakanusha nyota. Ama wale waliosema: ”Tumenyeshelezewa kwa sababu ya nyota kadhaa na kadhaa” anaamini nyota na amenikanusha Mimi.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Imesemekana kwamba kuomba du´aa wakati wa kunyesha mvua ni jambo lililopendekezwa.
´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
”Wakati Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipokuwa anaona mvua, husema:
اللّهُمَّ صَيِّـباً نافِـعاً
“Ee Allaah! Iteremshe kwa wingi na iwe yenye manufaa!”[2]
Anas (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Mvua ilinyesha nasi tukiwa pamoja na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam). Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) akakunja nguo yake ili mvua impate. Tukasema: ”Ee Mtume wa Allaah, kwa nini umefanya hivo?” Akasema: ”Kwa sababu ndio punde imetoka kwa Mola wake.” [3]
Ameipokea Muslim.
[1] al-Bukhaariy (846, 1037 na 4147) na Muslim (71).
[2] al-Bukhaariy (1032).
[3] Muslim (898).
Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Abiy Bakr bin Qayyim-il-Jawziyyah (afk. 751)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Waabil as-Swayyib wa Raafi´-ul-Kalim at-Twayyib, uk. 320
Imechapishwa: 09/09/2025
https://firqatunnajia.com/wakati-mvua-inanyesha/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket