Swali: Nini maana ya kwamba tawbah inakubaliwa muda wa kuwa mtu hajasagasaga miguu?
Jibu: Maana yake ni kwamba muda wa kuwa haujafika muda wa kukata roho baada ya kumuona Malaika wa kifo.
Swali: Vipi kuhusu maneno yake Fir´awn:
حَتَّىٰ إِذَا أَدْرَكَهُ الْغَرَقُ قَالَ آمَنتُ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا الَّذِي آمَنَتْ بِهِ بَنُو إِسْرَائِيلَ وَأَنَا مِنَ الْمُسْلِمِينَ
”… mpaka ilipomfikia kuzama akasema: ”Nimeamini kwamba hapana mungu wa haki, isipokuwa Yule waliyemwamini wana wa israaiyl, na mimi ni miongoni mwa waislamu.”[1]?
Jibu: Imani yake hii haikumfaa kitu kwa sababu adhabu imeshashuka. Amesema (Ta´ala):
فَلَمَّا رَأَوْا بَأْسَنَا قَالُوا آمَنَّا بِاللَّـهِ وَحْدَهُ وَكَفَرْنَا بِمَا كُنَّا بِهِ مُشْرِكِينَ فَلَمْ يَكُ يَنفَعُهُمْ إِيمَانُهُمْ لَمَّا رَأَوْا بَأْسَنَا
”Walipoiona adhabu Yetu walisema: ”Tumemuamini Allaah pekee na tunayakanusha vile ambavyo tulikuwa tunamshirikisha Naye. Haikuwa imani yao ni yenye kuwafaa pale walipoona adhabu Yetu.”[2]
Adhabu inaposhuka tawbah hainufaishi. Wakati kina Thaamuud na kina ´Aad walipoteremkiwa na adhabu tawbah haikuwanufaisha kitu. Tawbah inakubaliwa kabla ya hapo.
[1] 10:90
[2] 40:84-85
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24572/معنى-تقبل-التوبة-ما-لم-يغرغر
- Imechapishwa: 04/11/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
Related
68. Dalili kwamba kurejea kwa Allaah ni ´ibaadah na muda ambao tawbah inakubaliwa kutoka kwa mja
Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema: Dalili ya kurejea ni Kauli Yake (Ta´ala): وَأَنِيبُوا إِلَىٰ رَبِّكُمْ وَأَسْلِمُوا لَهُ مِن قَبْلِ أَن يَأْتِيَكُمُ الْعَذَابُ ثُمَّ لَا تُنصَرُونَ “Rejeeni kwa Mola wenu na jisalimisheni Kwake kabla haijakufikieni adhabu kisha hamtonusuriwa.”[1] MAELEZO Kurejea kuna maana ya kutubia. Kurejea na kutubia maana zake…
In "Sharh Thalaathat-il-Usuwl – al-Fawzaan"
20. Allaah ameizuia tawbah ya mzushi
Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema: Kwa ajili hii jopo la Salaf, akiwemo ath-Thawriy (Rahimahumu Allaah), wamesema: “Bid´ah ni yenye kupendeza zaidi kwa Ibliys kuliko maasi.” Kwa sababu maasi mtu hutubia kwayo. Bid´ah mtu hatubii kwayo. Hii ndio maana ya yale yaliyopokelewa na jopo katika wao kwamba: “Hakika Allaah amezuia…
In "Sharh Fadhwl-il-Islaam - Ibn Baaz"
10. Sharti za tawbah
Tawbah ya kweli iliyoamrishwa na Allaah ina sharti tano. Nazo ni kama ifuatavyo: 1 – Ikhlaasw. Tawbah yake iwe takasifu kwa ajili ya Allaah. Atubie dhambi kwa ajili ya kumtii Allaah (´Azza wa Jall), kumpenda, kumtukuza, kutaraji thawabu na kuogopa adhabu Yake. 2 – Aache maasi aliyokuwa akiyafanya. Ikiwa ni…
In "01. Kumi la mwisho la Ramadhaan"