Swali: Je, akemewe mwanamke ambaye anafunua uso wake mbele ya wanaume wa kando naye? Wanawake hawa wanachukua baadhi ya maneno ya wanazuoni wanaosema kuwa kuna makinzano kati ya wanazuoni kuhusu mwanamke kufunua uso wake.
Jibu: Kwa njia ya kumnasihi.
Swali: Wanasema kuwa wao wanachukua maoni ya fulani.
Jibu: Allaah (Jalla wa ´Alaa) amesema:
وَإِذَا سَأَلْتُمُوهُنَّ مَتَاعًا فَاسْأَلُوهُنَّ مِن وَرَاءِ حِجَابٍ ۚ ذَٰلِكُمْ أَطْهَرُ لِقُلُوبِكُمْ وَقُلُوبِهِنَّ
“Mnapowauliza basi waulizeni nyuma ya pazia. Hivyo ni utwaharifu zaidi kwa nyoyo zenu na nyoyo zao.” (33:53)
وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا لِبُعُولَتِهِنَّ أَوْ آبَائِهِنَّ
“Na wasidhihirishe mapambo yao isipokuwa kwa waume zao, au baba zao… ” (24:31)
Uso ndio pambo kubwa.
Swali: Je, wakatazwe?
Jibu: Wakatazwe, lakini iwe kwa upole na sio kwa ukali. Wapewe nasaha.
Swali: Kuhusu makinzano kuhusu kufunika uso kwa wanawake, ni maoni yepi yenye nguvu zaidi – kufunika au kufunua?
Jibu: Maoni yenyee nguvu ni kufunika kwa dalili ya Qur-aan.
Swali: Qur-aan imefuta suala la kufunua au kusemwe nini?
Jibu: Qur-aan imebainika kuwa ni wajibu kujisitiri. Mwanzoni wanawake walikuwa wakiruhusiwa kujifunua kisha baadaye Allaah akakataza hilo na kulifuta na kukabaki suala la kujisitiri.
Swali: Kwa hivyo ni lazima kujifunika?
Jibu: Ndio.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24627/كيف-تكون-النصيحة-لمن-تكشف-وجهها
- Imechapishwa: 15/11/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
Related
Maoni yanayosema inafaa kwa mwanamke kuacha wazi uso wake ni dhaifu
Swali: Wako wanazuoni wanaosema kuwa uso wa mwanamke sio uchi. Jibu: Haya ni maoni dhaifu na ni kosa. Swali: Wanajengea hoja kwa baadhi ya Hadiyth. Jibu: Hapana. Hadiyth inayosema mwanamke asivae Niqaab ni katika Ihraam. Wakati wa Ihraam hatakiwi kuvaa Niqaab na akavaa Niqaab inayoonyesha macho mawili. Hata hivyo anatakiwa…
In "Hajj na ´Umrah ya mwanamke"
Anajifungua kitambo kidogo baada ya kufariki kwa mume
Swali: Je, eda ya mwanamke mjamzito inakwisha akijifungua punde tu baada ya mume wake kuaga dunia? Jibu: Akijifungua kitambo kidogo tu baada kufariki mume wake, imemalizika eda yake: وَأُولَاتُ الْأَحْمَالِ أَجَلُهُنَّ أَن يَضَعْنَ حَمْلَهُنَّ ”Na wenye mimba muda wao [wa eda] watakapozaa mimba zao.”[1] Aayah hii ni kwa njia ya…
In "Eda"
Talaka ya mwenye hedhi
Swali: Mwanamme akimtaliki mke wake ndani ya hedhi talaka inapita au haikupita? Jibu: Ikiwa yeye mwanamme anajua hilo na mwanamke anajua hilo, maoni sahihi ni kwamba haipitiki kwa mtazamo wa baadhi ya wanazuoni. Wanazuoni wengi wanaona kuwa inapita. Lakini maoni sahihi zaidi ni kwamba haipiti kutokana na Hadiyth ya Ibn…
In "Talaka"