Swali: Kuhusu jitihada katika kufahamu maandiko, kwa sababu huenda mtu akaletewa maandiko bila ufahamu, nayo yanaweza kuwa maalum, ya ujumla, yasiyofungwa, yaliyofungwa, yenye kufuta au yaliyofutwa?

Jibu: Maandiko yanafahamika kwa kufuata kanuni za elimu. Lazima yafahamike kwa mujibu wa kanuni zinazojulikana ambazo zimewekwa na wanazuoni, kama vile kuunganisha maandiko yasiyofungwa na yale yenye kufungwa, kubainisha yaliyokusudiwa kwa ujumla kwa kuyaelekeza kwenye maalum, kuchukua yenye kufutwa kutoka kwenye yenye kufuta. Haya ni mambo yanayojulikana katika misingi yake. Lakini maneno ya kusema kwamba “hakuna jitihada kunapokuwepo andiko” si sahihi. Haya ni makosa.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1349/كيفية-فهم-النصوص
  • Imechapishwa: 14/12/2025