Swali: Vipi tutakusanya kati ya yale yaliyopokelewa kuwa ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) alitembelea makaburi na Hadiyth zinazokataza jambo hilo?
Jibu: ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) hakuwa na desturi ya kutembelea makaburi. Alizuru kaburi la ndugu yake, kwa sababu alifariki akiwa mbali naye karibu na Makkah. Akasema:
“Lau ningalikuwepo wakati wa kufa kwako, nisingekutembelea.”
Maana yake kama ningeshuhudia mauti yako, nisingekuja kaburini. Hii inaonyesha kwamba kutembelea makaburi kwa wanawake si jambo limesuniwa, kwa sababu kama ingekuwa ni jambo linaloruhusiwa kwao, basi angezuru hata kama angemshuhudia wakati wa kufa. Isitoshe wanawake wakati wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wakati wa makhaliyfah hawakuwa wakitembelea al-Baqiy´ wala makaburi ya mashahidi. Hivyo ikaeleweka kuwa kwao matembezi ya makaburi hayakusuniwa.
Hekima – Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) ndiye anayejua zaidi – ni kwamba wanawake, kama walivyosema wanauzoni wa Nadwah, ni wenye udhaifu wa subira na wepesi wa kutingishwa na mambo. Kwa hiyo wakiruhusiwa kutembelea makaburi, huenda zikadhihirika hali za huzuni kupindukia, maombolezo ya aina ya kupiga mayowe, kujifunua au kujipamba kupita kiasi, mambo ambayo mwisho wake si wenye kusifiwa. Vilevile wao ni mtihani kwa wanaume. Kwa hekima ya Allaah (´Azza wa Jall) akawakataza wanawake kusindikiza jeneza na kuzuia kuyatembelea makaburi. Maana lau wangesindikiza jeneza, ingeleta fitina katika wale wanaoandamana na jeneza. Kwa sababu mara chache mwanamke hutimiza kikamilifu stara, Hijaab na kujihifadhi. Hali kadhalika wakizuru makaburi watakuwa katika mazingira yanayoweza kuchanganyika na wanaume, jambo linaloweza kuleta madhara na fitina. Waweza pia kutokana na udhaifu wa subira wakaanza kuomboleza kwa sauti, jambo linalomdhuru maiti. Au wakaonyesha baadhi ya sehemu za miili yao kama nywele na kuwatia kwenye mtihani wanaume walio hai, na pia kumdhuru maiti kwa maombolezo na kelele zao. Mola wako ni Mwenye hekima na ni Mjuzi zaidi.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1129/الجمع-بين-زيارة-عاىشة-القبور-وبين-النهي-عن-زيارتها
- Imechapishwa: 08/06/2026
Swali: Vipi tutakusanya kati ya yale yaliyopokelewa kuwa ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) alitembelea makaburi na Hadiyth zinazokataza jambo hilo?
Jibu: ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) hakuwa na desturi ya kutembelea makaburi. Alizuru kaburi la ndugu yake, kwa sababu alifariki akiwa mbali naye karibu na Makkah. Akasema:
“Lau ningalikuwepo wakati wa kufa kwako, nisingekutembelea.”
Maana yake kama ningeshuhudia mauti yako, nisingekuja kaburini. Hii inaonyesha kwamba kutembelea makaburi kwa wanawake si jambo limesuniwa, kwa sababu kama ingekuwa ni jambo linaloruhusiwa kwao, basi angezuru hata kama angemshuhudia wakati wa kufa. Isitoshe wanawake wakati wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wakati wa makhaliyfah hawakuwa wakitembelea al-Baqiy´ wala makaburi ya mashahidi. Hivyo ikaeleweka kuwa kwao matembezi ya makaburi hayakusuniwa.
Hekima – Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) ndiye anayejua zaidi – ni kwamba wanawake, kama walivyosema wanauzoni wa Nadwah, ni wenye udhaifu wa subira na wepesi wa kutingishwa na mambo. Kwa hiyo wakiruhusiwa kutembelea makaburi, huenda zikadhihirika hali za huzuni kupindukia, maombolezo ya aina ya kupiga mayowe, kujifunua au kujipamba kupita kiasi, mambo ambayo mwisho wake si wenye kusifiwa. Vilevile wao ni mtihani kwa wanaume. Kwa hekima ya Allaah (´Azza wa Jall) akawakataza wanawake kusindikiza jeneza na kuzuia kuyatembelea makaburi. Maana lau wangesindikiza jeneza, ingeleta fitina katika wale wanaoandamana na jeneza. Kwa sababu mara chache mwanamke hutimiza kikamilifu stara, Hijaab na kujihifadhi. Hali kadhalika wakizuru makaburi watakuwa katika mazingira yanayoweza kuchanganyika na wanaume, jambo linaloweza kuleta madhara na fitina. Waweza pia kutokana na udhaifu wa subira wakaanza kuomboleza kwa sauti, jambo linalomdhuru maiti. Au wakaonyesha baadhi ya sehemu za miili yao kama nywele na kuwatia kwenye mtihani wanaume walio hai, na pia kumdhuru maiti kwa maombolezo na kelele zao. Mola wako ni Mwenye hekima na ni Mjuzi zaidi.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1129/الجمع-بين-زيارة-عاىشة-القبور-وبين-النهي-عن-زيارتها
Imechapishwa: 08/06/2026
https://firqatunnajia.com/vipi-kuoanisha-kati-ya-makatazo-ya-wanawake-kuyatembelea-makaburi-na-kitendo-cha-aaishah-kumtembelea-ibn-awf/