Swali: Ni ipi hukumu ya kula nyama zinazotoka kwa Ahl-ul-Kitaab ilihali hali zao hazijulikani?
Jibu: Ikiwa wanachinja kwa njia ya Kishari´ah Allaah ametuhalalishia vichinjwa vyao. Na ikiwa hawachinji kwa njia ya Kishari´ah, na wewe ukawa unajua hili, usile. Hata muislamu akichinja kwa njia isiyokuwa ya Kishari´ah sio halali kula kichinjwa chake.
Kuhusiana na kichinjwa usichojua kama kinachinjwa kwa njia ya Kishari´ah au isiyokuwa ya Kishari´ah, bora zaidi jiepushe nacho kwa njia ya kujiepusha na yenye kutia mashaka.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Fath-il-Majiyd (26) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/fathul%20%20-%204%20-%201%20-%201436.mp3
- Imechapishwa: 11/02/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket