Swali: Ni ipi hukumu ya kufanya utani katika dini ya Uislamu? Je, ni jambo linaingia katika maneno ya upuuzi pamoja na kuzingatia kwamba haihusiani na kuchezea dini shere?
Jibu: Hapana vibaya kufanya utani kwa maneno muda wa kuwa ni kwa haki na ukweli khaswakhaswa ikiwa mtu hafanyi hivo kwa wingi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akifanya mzaha na hasemi isipokuwa ukweli mtupu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Lakini haijuzu ikiwa ni utani wa wongo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ole wa yule mwenye kuzungumza akadanganya ili awachekeshe watu! Ole wake! Kisha ole wake!”
Ameipokea Abu Daawuud, at-Tirmidhiy na an-Nasaa´iy kwa cheni ya wapokezi nzuri.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (06/391)
- Imechapishwa: 07/03/2021
Swali: Ni ipi hukumu ya kufanya utani katika dini ya Uislamu? Je, ni jambo linaingia katika maneno ya upuuzi pamoja na kuzingatia kwamba haihusiani na kuchezea dini shere?
Jibu: Hapana vibaya kufanya utani kwa maneno muda wa kuwa ni kwa haki na ukweli khaswakhaswa ikiwa mtu hafanyi hivo kwa wingi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akifanya mzaha na hasemi isipokuwa ukweli mtupu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Lakini haijuzu ikiwa ni utani wa wongo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ole wa yule mwenye kuzungumza akadanganya ili awachekeshe watu! Ole wake! Kisha ole wake!”
Ameipokea Abu Daawuud, at-Tirmidhiy na an-Nasaa´iy kwa cheni ya wapokezi nzuri.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (06/391)
Imechapishwa: 07/03/2021
https://firqatunnajia.com/utani-na-mzaha-katika-uislamu/