Swali: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Kutabasamu usoni mwa ndugu yako ni swadaqah.”
Je, hii ni dalili ya kwamba mtu asitabasamu usoni mwa mshirikina au kafiri?
Jibu: Mshirikina inatakiwa kumuonyesha ushupavu, chuki na kumdhihirishia kujitenga. Mapenzi, tabasamu na ushirikiano yanakuwa kati ya waislamu. Hayo yanakuwa baina ya waislamu. Lakina kwa makafiri ni chuki, bughudha na uadui; isipokuwa wakati mtu anatarajia manufaa kama vile kuzilainisha nyoyo zao kwa ajili ya kuwalingania kwa Allaah. Katika hali hiyo hapana vibaya.
Swali: Kwa hiyo inafaa kutabasamu usoni mwake kwa ajili ya kumlingania katika dini ya Allaah?
Jibu: Hapana vibaya. Hapana vibaya kwa ajili ya kumlingania kwa Allaah pale atakapoona manufaa ya kufanya hivo.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24596/حكم-التبسم-في-وجه-الكافر-للدعوة
- Imechapishwa: 08/11/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)