Swali: Kuna mtu amewazuia watu njia kwa gari yake, ambapo akaja mtu na kumlaani kutokana na maudhi aliyosababisa, na kwa ajili hiyo anastahiki kulaaniwa. Je, ni sahihi?
Jibu: Ndio. Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
”Bwana mmoja alisema: ”Ee Mtume wa Allaah! Kuna jirani anayeniudhi.” Akasema: ”Nenda utoe samani zako barabarani.” Akaenda na kutoa samani zake njiani. Watu wakamkusanyikia na kusema: ”Una nini wewe?” Akasema: ”Nina jirani anayeniudhi. Nikamweleza hilo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), ambaye akasema: ”Nenda utoe samani zako barabarani.” Ndipo wakaanza kusema: ”Ee Allaah, mlaani! Ee Allaah, mfedheheshe!” Alipofikiwa na khabari hiyo, akamwendea na kusema: ”Rejea nyumbani kwako. Naapa kwa Allaah sintokuudhi!”[1]
Yeye mwenyewe ndiye kasababisha. Hiyo ni adhabu yake.
[1] al-Adab al-Mufrad (124). Nzuri na Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (41)
- Imechapishwa: 28/06/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)