Wanazuoni waliofeli hawawaelekezi watu katika kheri. Wanachojali ni manufaa yao. Wakati tulipokuwa tunasoma katika chuo kikuu cha Kiislamu, kuna mwalimu wetu mmoja alitwambia:

“Enyi wanangu vipenzi! Msiharamishe picha. Mkiharamisha picha basi mtawaweka watu katika uzito.”

Ametakasika Allaah na mapungufu! Masikini! Sisi ndio wenye haki ya kuhalalisha na kuharamisha au ni Allaah (´Azza wa Jall)? Sisi hatuna la kusema. Hatuwezi kusema jambo fulani kuwa ni halali au haramu pasi na dalili kutoka ndani ya Qur-aan na Sunnah. Je, sisi ni wenye huruma zaidi juu ya waja wa Allaah kuliko Allaah ambaye amesema:

وَمَا كَانَ رَبُّكَ نَسِيًّا

“Mola wako si Mwenye kusahau kabisa?”[1]

Si ingeliwezekana kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kusema:

“Allaah amewalaani watengeneza picha – isipokuwa katika zama za mwisho.”

Si angeliweza kusema:

“Malaika hawaingii nyumba ilio na picha – isipokuwa katika zama za mwisho.”

Miongoni mwa ujanja wa wafeliji hawa, ambao daima hujilinda kwa maoni. Sisi tunawaambia:

“Yule anayemwamini Allaah na siku ya Mwisho basi azungumze kheri au anyamaze.”[2]

Ni lazima kuwatambua Ahl-us-Sunnah na Kundi lililookoka ili uwaulize kuhusu dini hii.

[1] 19:64

[2] al-Bukhaariy na Muslim.

  • Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 313
  • Imechapishwa: 19/05/2025