Swali: Pindi ninaposwali Dhuhaa na nikasubiri Dhuhr huzidiwa na ulalaji. Je, wudhuu´ wangu unachenguka?
Jibu: Kusinzia hakuchengui wudhuu´. Kinachochengua ni kulala ambako mtu hahisi yanayoendelea pambizoni mwake. Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) kipindi cha Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) walikuwa wanasubiri ´Ishaa ambapo vichwa vyao vinainama kutokana na kusinzia kisha wanainuka na wala hawatawadhi. Kuhusu usingizi mzito ambao unaondosha hisia unachengua wudhuu´. Kwa hivyo, ee dada kwa ajili ya Allaah, unatakiwa kutambua tofauti kati ya usingizi mzito unaoondosha zile hisia na kulala.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (10/142)
- Imechapishwa: 20/08/2021
Swali: Pindi ninaposwali Dhuhaa na nikasubiri Dhuhr huzidiwa na ulalaji. Je, wudhuu´ wangu unachenguka?
Jibu: Kusinzia hakuchengui wudhuu´. Kinachochengua ni kulala ambako mtu hahisi yanayoendelea pambizoni mwake. Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) kipindi cha Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) walikuwa wanasubiri ´Ishaa ambapo vichwa vyao vinainama kutokana na kusinzia kisha wanainuka na wala hawatawadhi. Kuhusu usingizi mzito ambao unaondosha hisia unachengua wudhuu´. Kwa hivyo, ee dada kwa ajili ya Allaah, unatakiwa kutambua tofauti kati ya usingizi mzito unaoondosha zile hisia na kulala.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (10/142)
Imechapishwa: 20/08/2021
https://firqatunnajia.com/usingizi-unaochengua-wudhuu-na-usiochengua/