Swali: Haijuzu kwa mume kumzuia mkewe kwenda msikitini?

Jibu: Ndio, hana haki ya kumzuia. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Msiwazuie… “

Haifai kwake kumuasi Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

Swali: Vipi akimzuia kwa haja kwa mfano kuwalea watoto wake au kusimamia kazi ya nyumbani?

Jibu: Hapana:

”Msiwazuie wajakazi wa Allaah kutokana na misikiti ya Allaah. Hata hivyo nyumba zao ni bora kwao.”[1]

[1] Ahmad (2/76) na Abu Daawuud (567). Imesahihishwa na Ibn Khuzaymah (1684) na al-Haakim (755).

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23921/هل-يجوز-منع-الزوجة-من-الذهاب-للمسجد
  • Imechapishwa: 31/05/2024