Usiitikie ”Aamiyn” kwa sauti ya juu wakati wa du´aa ya imamu siku ya ijumaa

Swali: Imamu anapokuwa anaomba du´aa mwishoni mwa Khutbah watu wengi huitikia ”Aamiyn” baada ya du´aa yake. Je, hili linahesabiwa kuwa ni katika maneno na kufanya upuuzi ndani ya Khutbah?

Jibu: Hapana, hakuna tatizo. Kila mtu aitikie ”Aamiyn” baina yake na nafsi yake pasi na kuleta usumbufu. Ni kama kuitikia ”Aamiyn” katika du´aa ya Qunuut.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31000/ما-حكم-التامين-على-الدعاء-في-خطبة-الجمعة
  • Imechapishwa: 20/09/2025