Swali: Mwanamume anaruhusiwa nini kutoka kwa mke wake katika siku za hedhi?
Jibu: Mwanamume anaruhusiwa kutoka kwa mke wake kila kitu isipokuwa tendo la ndoa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Fanyeni kila kitu isipokuwa tendo la ndoa.”
Wakati alipoambiwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba mayahudi hawakai na mwanamke anapokuwa katika hedhi majumbani, hawakai nao majumbani, hawali pamoja nao wala hawanywi nao. Ndipo akasema (´alayhis-Salaam):
”Fanyeni kila kitu isipokuwa tendo la ndoa.”
Allaah ameteremsha kuhusu hilo:
وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الْمَحِيضِ ۖ قُلْ هُوَ أَذًى فَاعْتَزِلُوا النِّسَاءَ فِي الْمَحِيضِ ۖ وَلَا تَقْرَبُوهُنَّ حَتَّىٰ يَطْهُرْنَ
“Wanakuuliza kuhusu hedhi. Sema: “Hiyo ni dhara, hivyo basi waepukeni wanawake katika hedhi. Wala msiwakaribie kujimai nao mpaka watwaharike.”[1]
Kwa maana ya jimaa.
Kuhusu kulala naye, kumkumbatia, kumbusu na mengineyo, hakuna tatizo lolote. Isipokuwa tendo la ndoa pekee.
´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) alikuwa anakunywa kutoka kwenye chombo, kisha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anakichukua na kuweka mdomo wake pale alipoweka mdomo wake. Pia alikuwa anakula kipande cha mfupa kilichokuwa na nyama, naye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anakichukua na kula katika sehemu aliyokula, ili kutuliza moyo wake, kumfariji na kumtania kwa upole (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
[1] 02:222
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/30118/ماذا-يجوز-للرجل-من-زوجته-ايام-الحيض
- Imechapishwa: 12/09/2025
Swali: Mwanamume anaruhusiwa nini kutoka kwa mke wake katika siku za hedhi?
Jibu: Mwanamume anaruhusiwa kutoka kwa mke wake kila kitu isipokuwa tendo la ndoa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Fanyeni kila kitu isipokuwa tendo la ndoa.”
Wakati alipoambiwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba mayahudi hawakai na mwanamke anapokuwa katika hedhi majumbani, hawakai nao majumbani, hawali pamoja nao wala hawanywi nao. Ndipo akasema (´alayhis-Salaam):
”Fanyeni kila kitu isipokuwa tendo la ndoa.”
Allaah ameteremsha kuhusu hilo:
وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الْمَحِيضِ ۖ قُلْ هُوَ أَذًى فَاعْتَزِلُوا النِّسَاءَ فِي الْمَحِيضِ ۖ وَلَا تَقْرَبُوهُنَّ حَتَّىٰ يَطْهُرْنَ
“Wanakuuliza kuhusu hedhi. Sema: “Hiyo ni dhara, hivyo basi waepukeni wanawake katika hedhi. Wala msiwakaribie kujimai nao mpaka watwaharike.”[1]
Kwa maana ya jimaa.
Kuhusu kulala naye, kumkumbatia, kumbusu na mengineyo, hakuna tatizo lolote. Isipokuwa tendo la ndoa pekee.
´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) alikuwa anakunywa kutoka kwenye chombo, kisha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anakichukua na kuweka mdomo wake pale alipoweka mdomo wake. Pia alikuwa anakula kipande cha mfupa kilichokuwa na nyama, naye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anakichukua na kula katika sehemu aliyokula, ili kutuliza moyo wake, kumfariji na kumtania kwa upole (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
[1] 02:222
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/30118/ماذا-يجوز-للرجل-من-زوجته-ايام-الحيض
Imechapishwa: 12/09/2025
https://firqatunnajia.com/unayoruhusiwa-kufanya-na-mwanamke-kipindi-cha-hedhi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
