Abu Humayd, au Abu Usayd, ameeleza ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

48 – Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akisema wakati anapoingia Msikitini:

“Mmoja wenu anapoingia Msikitini amswalie Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na aseme:

اللهُمَّ افْتَحْ لِي أَبْوَابَ رَحْمَتِكَ

“Allaah! Nifungulie milango ya rehema Zako.”

Wakati anapotoka aseme:

اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ مِنْ فَضْلِكَ

“Allaah! Ninakuomba kutoka katika fadhilah Zako.”[1]

Ameipokea Muslim.

´Abdullaah bin ´Amr (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesimulia ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa wakati anapoingia msikitini husema:

أَعُوذُ باللهِ الْعَظِيم وَبِوَجْهِهِ الْكَرِيمِ وَبِسُلْطَانِهِ الْقَدِيمِ مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيمِ

“Najikinga na Allaah, Mtukufu, na kwa uso Wake mtukufu na kwa utawala Wake wa milele kutokana na shaytwaan aliyefukuzwa mbali na rehema za Allaah.”

Akasema:

”Akisema hivo shaytwaan husema: ”Amehifadhiwa dhidi yangu siku iliobaki.”[2]

Ameipokea Abu Daawuud.

[1] Muslim (713).

[2] Abu Daawuud (466). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Swahiyh Sunan Abiy Daawuud” (466).

  • Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Abiy Bakr bin Qayyim-il-Jawziyyah (afk. 751)
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Waabil as-Swayyib wa Raafi´-ul-Kalim at-Twayyib, uk. 264
  • Imechapishwa: 17/09/2025