Swali: Ni ipi hukumu ya kuuliza matukio kabla ya kutokea kwake?
Jibu: Ikiwa yanamuhusu na kwa ajili hiyo anachela juu yake ayaulize. Makatazo yalikuwa katika zama za Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hii leo mambo yamethibiti na hivyo mtu aulize yale anayoyahitajia. Lakini katika zama za Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) imekatazwa:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَسْأَلُوا عَنْ أَشْيَاءَ إِن تُبْدَ لَكُمْ تَسُؤْكُمْ
“Enyi mlioamini! Msiulizie mambo ambayo mkidhihirishiwa yatakuchukizeni.” (05:101)
Akae kimya isipokuwa kuuliza yale yanayomuhusu. Kuhusu leo Shari´ah imeshathibiti. Mambo ya wajibu na mambo ya haramu yameshathibiti. Kwa hivyo hapana vibaya akiuliza kuhusu yale mambo anayochelea kuyaingia au yale mambo ya wajibu ambayo yamejificha kwake, kwani Shari´ah imeshathibiti.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh al-Arba´iyn an-Nawawiyyah (09)
- Imechapishwa: 05/11/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)