2925 – ´Abdullaah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) analala ilihali amesujudu, kulala kwake hakutambuliki isipokuwa pale anapokoroma. Halafu anasimama na kuendelea na swalah yake.”
Ameipokea Ibn Abiy Shaybah katika ”al-Muswannaf” na kupitia kwake al-Baghawiy katika ”Sharh-us-Sunnah”: Ishaaq bin Mansuur ametuhadithia, kutoka kwa Mansuur bin Abiyl-Aswad, kutoka kwa al-A´mash, kutoka kwa Ibraahiym, kutoka kwa ´Alqamah, kutoka kwa ´Abdullaah.
Cheni ya wapokezi wake ni Swahiyh. Wapokezi wake ni waaminifu na ni wapokezi wa al-Bukhaariy na Muslim isipokuwa tu Mansuur bin Abiyl-Aswad, lakini na yeye pia ni mwaminifu.
Ibn Abiy Shaybah pia ameihadithia pasi na Swahabah katika cheni ya wapokezi: Hushaym ametuhadithia, kutoka kwa Mughiyrah, kutoka kwa Ibraahiym ambaye amesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alilala katika msikiti mpaka akakoroma. Halafu akasimama na kuswali na wala hakutawadha. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yalikuwa yanalala macho yake na wala haulali moyo wake.”
Kisha Ibn Abiy Shaybah na Ahmad wakasema: Wakiy´ ametuhadithia, kutoka kwa al-A´mash, kutoka kwa Ibraahiym, kutoka kwa al-Aswad, kutoka kwa ´Aaishah aliyesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akilala mpaka anakoroma. Kisha anasimama na kuswali na wala hatawadhi.”
Cheni ya wapokezi ni Swahiyh kwa mujibu wa masharti ya al-Bukhaariy na Muslim. Kuhusu ziada ya Ibraahiym:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yalikuwa yanalala macho yake na wala haulali moyo wake.”
ni Swahiyh kwa cheni ya wapokezi ilioungana katika al-Bukhaariy na Muslim na kwenginepo. Nimeitoa katika ”Swahiyh Sunan Abiy Daawuud” (1212).
Ziada hii ni dalili ya wazi kabisa kwamba usingizi wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) haukuchengua wudhuu´ wake na kwamba sifa hiyo ni maalum kwake yeye. Wanachuoni wametofautiana kama wudhuu´ wa aliyelala ambaye yuko imara katika ukaaji wake unachenguka au hauchunguki. Maoni yenye nguvu ni kwamba unachenguka, kama nilivyobainisha katika ”Tamaam-ul-Minnah”.
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Silsilat-ul-Ahaadiyth as-Swahiyhah (6/2/1027-1028)
- Imechapishwa: 17/08/2020
2925 – ´Abdullaah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) analala ilihali amesujudu, kulala kwake hakutambuliki isipokuwa pale anapokoroma. Halafu anasimama na kuendelea na swalah yake.”
Ameipokea Ibn Abiy Shaybah katika ”al-Muswannaf” na kupitia kwake al-Baghawiy katika ”Sharh-us-Sunnah”: Ishaaq bin Mansuur ametuhadithia, kutoka kwa Mansuur bin Abiyl-Aswad, kutoka kwa al-A´mash, kutoka kwa Ibraahiym, kutoka kwa ´Alqamah, kutoka kwa ´Abdullaah.
Cheni ya wapokezi wake ni Swahiyh. Wapokezi wake ni waaminifu na ni wapokezi wa al-Bukhaariy na Muslim isipokuwa tu Mansuur bin Abiyl-Aswad, lakini na yeye pia ni mwaminifu.
Ibn Abiy Shaybah pia ameihadithia pasi na Swahabah katika cheni ya wapokezi: Hushaym ametuhadithia, kutoka kwa Mughiyrah, kutoka kwa Ibraahiym ambaye amesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alilala katika msikiti mpaka akakoroma. Halafu akasimama na kuswali na wala hakutawadha. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yalikuwa yanalala macho yake na wala haulali moyo wake.”
Kisha Ibn Abiy Shaybah na Ahmad wakasema: Wakiy´ ametuhadithia, kutoka kwa al-A´mash, kutoka kwa Ibraahiym, kutoka kwa al-Aswad, kutoka kwa ´Aaishah aliyesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akilala mpaka anakoroma. Kisha anasimama na kuswali na wala hatawadhi.”
Cheni ya wapokezi ni Swahiyh kwa mujibu wa masharti ya al-Bukhaariy na Muslim. Kuhusu ziada ya Ibraahiym:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yalikuwa yanalala macho yake na wala haulali moyo wake.”
ni Swahiyh kwa cheni ya wapokezi ilioungana katika al-Bukhaariy na Muslim na kwenginepo. Nimeitoa katika ”Swahiyh Sunan Abiy Daawuud” (1212).
Ziada hii ni dalili ya wazi kabisa kwamba usingizi wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) haukuchengua wudhuu´ wake na kwamba sifa hiyo ni maalum kwake yeye. Wanachuoni wametofautiana kama wudhuu´ wa aliyelala ambaye yuko imara katika ukaaji wake unachenguka au hauchunguki. Maoni yenye nguvu ni kwamba unachenguka, kama nilivyobainisha katika ”Tamaam-ul-Minnah”.
Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Silsilat-ul-Ahaadiyth as-Swahiyhah (6/2/1027-1028)
Imechapishwa: 17/08/2020
https://firqatunnajia.com/ulalaji-wa-kukaa-unachengua-wudhuu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)