Swali: Je, watu wa Jeddah wana wajibu wa kufanya Twawaaf-ul-Wadaa´ na ni ipi dalili?
Jibu: Ndio, kwa kuwa wao si miongoni mwa watu wa Haram na wala hawako katika hukumu ya watu wa Haram. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Asiondoke yeyote miongoni mwenu mpaka mwisho wa kitendo chake kiwe ni kuiaga Nyumba.”
Ameipokea Muslim.
Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Watu wameamrishwa mwisho wa matendo yao iwe ni kuiaga Nyumba, isipokuwa amefanyiwa wepesi mwanamke mwenye hedhi.”
Kwa hiyo watu wa Jeddah na watu wa Twaa-if si miongoni mwa wakazi wa Makkah, si miongoni mwa watu wa Haram. Ikiwa watataka kuondoka baada ya Hajj, basi ni juu yao kufanya Twawaaf-ul-Wadaa´. Ama kuhusu ´Umrah, jambo lake ni pana na rahisi zaidi. Wakifanya Twawaaf-ul-Wadaa´ ndio bora zaidi. Wakiacha, basi yaliyo sahihi ni kwamba si lazima kuaga katika ´Umrah. Hata hivyo ni lazima katika Hajj kwa mujibu wa maoni sahihi.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/30132/هل-على-اهل-جدة-طواف-وداع-وما-الدليل
- Imechapishwa: 12/09/2025
Swali: Je, watu wa Jeddah wana wajibu wa kufanya Twawaaf-ul-Wadaa´ na ni ipi dalili?
Jibu: Ndio, kwa kuwa wao si miongoni mwa watu wa Haram na wala hawako katika hukumu ya watu wa Haram. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Asiondoke yeyote miongoni mwenu mpaka mwisho wa kitendo chake kiwe ni kuiaga Nyumba.”
Ameipokea Muslim.
Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Watu wameamrishwa mwisho wa matendo yao iwe ni kuiaga Nyumba, isipokuwa amefanyiwa wepesi mwanamke mwenye hedhi.”
Kwa hiyo watu wa Jeddah na watu wa Twaa-if si miongoni mwa wakazi wa Makkah, si miongoni mwa watu wa Haram. Ikiwa watataka kuondoka baada ya Hajj, basi ni juu yao kufanya Twawaaf-ul-Wadaa´. Ama kuhusu ´Umrah, jambo lake ni pana na rahisi zaidi. Wakifanya Twawaaf-ul-Wadaa´ ndio bora zaidi. Wakiacha, basi yaliyo sahihi ni kwamba si lazima kuaga katika ´Umrah. Hata hivyo ni lazima katika Hajj kwa mujibu wa maoni sahihi.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/30132/هل-على-اهل-جدة-طواف-وداع-وما-الدليل
Imechapishwa: 12/09/2025
https://firqatunnajia.com/twawaaf-ul-wadaa-kwa-wakazi-wa-jeddah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket