Twawaaf-ul-Wadaa´ kwa anayefanya ´Umrah

Swali: Vipi kuhusu Twawaaf-ul-Wadaa´ kwa mwenye kufanya ´Umrah?

Jibu: Maoni sahihi ni kwamba Twawaaf-ul-Wadaa´ kwa mwenye kufanya ´Umrah ni wajibu. Isipokuwa ikiwa mtu anarudi kutoka safari yake papohapo kwa njia ya kwamba ametufu, akafanya Sa´y, akapunguza kisha akapanda gari yake na kurudi. Huyu itamtosha ile Twawaaf ya kwanza. Ama akibaki, japo saa moja tu, basi ni lazima kwake kufanya Twawaaf-ul-Wadaa´ wakati wa kutoka.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Liqaa´ ash-Shahriy (77) http://binothaimeen.net/content/1776
  • Imechapishwa: 19/09/2020