Swali: Allaah (Ta´ala) amesema:
لَا يَسْتَأْذِنُكَ الَّذِينَ يُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ أَن يُجَاهِدُوا بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ ۗ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِالْمُتَّقِينَ
“Hawakuombi ruhusa [ya kubakia nyuma] wale waliomwamini Allaah na Siku ya Mwisho wasifanye jihaad kwa mali zao na nafsi zao. Na Allaah ni Mjuzi kwa wachaji.” (09:44)
Kuna ambao wanatumia Aayah hii kama dalili juu ya kujuzu kutoka kwenda katika Jihaad bila ya idhini ya kiongozi. Ni ipi maana ya Aayah hii? Je, dalili hii…
Jibu: Ametakasika Allaah! Allaah amesema:
لَا يَسْتَأْذِنُكَ
“Hawakuombi ruhusa [ya kubakia nyuma]… “
Ni nani mwenye kuombwa idhini? Ni nani ambaye Allaah (Jalla wa ´Alaa) anamzungumzisha? Ni dalili yenye kuonesha kuwa mtawala ndiye mwenye kutoa idhini ya Jihaad au kutoitoa. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ndiye ambaye alikuwa mtawala. Leo hii viongozi baada yake. Tazama dalili hii iliyopinda! Wanatumia hoja kwa dalili ilio dhidi yao:
لَا يَسْتَأْذِنُكَ
“Hawakuombi ruhusa [ya kubakia nyuma] wale… “
Ni dalili yenye kuonesha kuwa yule mwenye kutakwa idhini juu ya Jihaad au kutokuwepo Jihaad kwa sababu ya udhuru ilikuwa ni Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Yeye ndiye aliyekuwa kiongozi. Vivyo hivyo wale watawala wa waislamu waliokuja baada yake.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Tafsiyr-ish-Shaykh Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (23) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tafsirayat-12-07-1435-01_0.mp3
- Imechapishwa: 19/06/2020
Swali: Allaah (Ta´ala) amesema:
لَا يَسْتَأْذِنُكَ الَّذِينَ يُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ أَن يُجَاهِدُوا بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ ۗ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِالْمُتَّقِينَ
“Hawakuombi ruhusa [ya kubakia nyuma] wale waliomwamini Allaah na Siku ya Mwisho wasifanye jihaad kwa mali zao na nafsi zao. Na Allaah ni Mjuzi kwa wachaji.” (09:44)
Kuna ambao wanatumia Aayah hii kama dalili juu ya kujuzu kutoka kwenda katika Jihaad bila ya idhini ya kiongozi. Ni ipi maana ya Aayah hii? Je, dalili hii…
Jibu: Ametakasika Allaah! Allaah amesema:
لَا يَسْتَأْذِنُكَ
“Hawakuombi ruhusa [ya kubakia nyuma]… ”
Ni nani mwenye kuombwa idhini? Ni nani ambaye Allaah (Jalla wa ´Alaa) anamzungumzisha? Ni dalili yenye kuonesha kuwa mtawala ndiye mwenye kutoa idhini ya Jihaad au kutoitoa. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ndiye ambaye alikuwa mtawala. Leo hii viongozi baada yake. Tazama dalili hii iliyopinda! Wanatumia hoja kwa dalili ilio dhidi yao:
لَا يَسْتَأْذِنُكَ
“Hawakuombi ruhusa [ya kubakia nyuma] wale… ”
Ni dalili yenye kuonesha kuwa yule mwenye kutakwa idhini juu ya Jihaad au kutokuwepo Jihaad kwa sababu ya udhuru ilikuwa ni Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Yeye ndiye aliyekuwa kiongozi. Vivyo hivyo wale watawala wa waislamu waliokuja baada yake.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Tafsiyr-ish-Shaykh Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (23) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tafsirayat-12-07-1435-01_0.mp3
Imechapishwa: 19/06/2020
https://firqatunnajia.com/tazama-dalili-hii-iliyopinda/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)