Swali: Kuomba Du´aa kwa haki ya fulani au kwa jaha ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) au kwa dhati ya viumbe ni njia inayopelekea katika shirki au ni shirki kabisa?
Jibu: Ni Bid´ah. Kuomba Du´aa kwa jaha au kwa haki ya fulani ni Bid´a. Ni njia inayopelekea katika shirki. Ni jambo limekusanya mambo mawili:
1- Ni Bid´ah. Kwa kuwa ni kufanya jambo lisilokuwa na dalili kutoka katika Qur-aan na Sunnah.
2- Ni njia pia inayopelekea katika shirki. Waabudu makaburi hawakutumbukia katika kuyaabudu makaburi isipokuwa ilikuwa ni kwa sababu ya hili. Walianza kwa kutawassul kwao kwanza kisha ndio wakajikurubisha kwao kwa kuwafanyia ´ibaadah na utiifu. Hivyo wakawa wametumbukia kwenye shirki kubwa.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Aqiydat-is-Saffaariniyyah (13) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/sfranih_13.mp3
- Imechapishwa: 18/06/2018
Swali: Kuomba Du´aa kwa haki ya fulani au kwa jaha ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) au kwa dhati ya viumbe ni njia inayopelekea katika shirki au ni shirki kabisa?
Jibu: Ni Bid´ah. Kuomba Du´aa kwa jaha au kwa haki ya fulani ni Bid´a. Ni njia inayopelekea katika shirki. Ni jambo limekusanya mambo mawili:
1- Ni Bid´ah. Kwa kuwa ni kufanya jambo lisilokuwa na dalili kutoka katika Qur-aan na Sunnah.
2- Ni njia pia inayopelekea katika shirki. Waabudu makaburi hawakutumbukia katika kuyaabudu makaburi isipokuwa ilikuwa ni kwa sababu ya hili. Walianza kwa kutawassul kwao kwanza kisha ndio wakajikurubisha kwao kwa kuwafanyia ´ibaadah na utiifu. Hivyo wakawa wametumbukia kwenye shirki kubwa.
Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh ´Aqiydat-is-Saffaariniyyah (13) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/sfranih_13.mp3
Imechapishwa: 18/06/2018
https://firqatunnajia.com/tawassul-za-bidah-zinapelekea-katika-shirki/